SIRI YA UPONYAJI
SOMO: SIRI YA KUPONYWA UTANGULIZI Tunaposema juu ya uponyaji na kufanikiwa haina maana juu ya uponyaji wa aina moja tu, yaani uponyaji wa mwili tu. Biblia inaposema uponyaji ina maana katika maeneo matatu yaani; 1. Uponyaji wa Rohoni 2. Uponyaji wa Nafsi 3. Uponyaji wa Mwili 3 Yohana 1:1 – 2 “Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli. Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo” Efeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa Baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo”. Zaburi 103:3 – 5 “Akusamehe maovu yako yote, akuponya magonjwa yako yote, aukomboa uhai wako na kaburi, akutia taji ya fadhili na rehema, aushibisha mema uzee wako, ujana wako ukarejezwa kama tai” 2 Petro 3:17 “Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuucha uthabiti wenu”. 2 Katika maandiko hayo uaona kuna maeneo matatu yahusuyo up...