SOMO: HUDUMA

Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye Yule”. 1 Wakorintho 12 :5

HUDUMA NI NINI?

Huduma ni kazi ambayo mtu hupewa/kapewa na Mungu aifanye kwa uongozi wa Roho Mtakatifu  kwa ajili ya kuwafanya watu wamjue Mungu na kudumu katika maisha matakatifu ili wawe na uzima wa milele.

Huduma ni kazi apewayo mtu na Roho wa Mungu ili apeleke ujumbe wa Mungu kwa watu.

Mfano 1. Utume 2. Unabii 3. Uchungaji 4. Uinjilisti 5. Ualimu

Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye Yule”. 1 Wakorintho 12 :5

Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, *wa kwanza mitume* , wa *pili manabii* , *wa tatu waalimu,* kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha. Je! *Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu?* Wote wanatenda miujiza? 1 Wakorintho 12:2829

Huduma ni kazi ya Kiroho

Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; Waefeso 4:11

Huduma ni wito ambao mtu huitwa na Mungu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Yeremia 1:5. Mungu alimjua Yeremia tangu tumboni mwa mamaye. Pia alimjua Yohana tangu tumboni mwa mamaye.
Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana. Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake. Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye. Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.  Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa. Luka 1:13 - 17

KARAMA ZA HUDUMA TANO (Efeso. 4:11)

Katika kitabu cha Waefeso 4:11 Mtume Paulo ameweka wazi huduma katika nafasi Tano na lengo za huduma hizi katika kanisa ni KUWAKAMILISHA WATAKATIFU HATA MWILI WA KRISTO UPATE KUJENGWA.

Mwili wa Kristo ni KANISA.

1.      Huduma ya Utume/Mtume

a)     Mtume (Gk. Apostolos = aliyetumwa / pelekwa.

Neno hili Lilitumika kuelezea au kuwakilisha;

i. Balozi

ii. Kikundi cha merikebu kilichopelekwa ili kuanzisha koloni jipya

iii. Nahodha anayeamuru merikebu hizo.

iv. Koloni lililoanzishwa na nahodha.

b)     Mtume ni mtu wa umisheni, Mwenye kumuwakilisha na kuyafanya mapenzi yake aliyempeleka/aliyemtuma. Ni asemaye na kutenda kwa niaba ya mwingine.

Yesu Kristo ndiye mwanzilishi wa Utume kwani alipelekwa na Baba yaani Mungu kuyafanya mapenzi ya Baba/ Mungu. YESU kama Mtume na Mitume Aliowaweka (Yoh. 6:38, 12:49 - 50)

Yesu Kristo aliwaweka Mitume  kwa kusudi au lengo

·        Wawe mabalozi/ Mitume –kumuwakilisha ulimwenguni

·        Waanzishe koloni jipya -  yaani Kanisa, Koloni la kifalme, lenye mamlaka ya Ufalme wa Mungu nyuma yake. Na hapo kwanza kanisa la kwanza liliitwa Kanisa la Mitume.

·        Ili kupata Kanisa ambalo mapenzi ya Mungu yanatimizwa ulimwenguni kama vile mbinguni. Yoh. 20:21, Mt.10:40; 16:18, Efe.2:20

Aina /Viwango Vya Mitume Katika Agano Jipya

Vipo viwango vya aina nne vya huduma ya Utume, kati yake viwili havitendi kazi tena kwa hivi sasa. Viwango hivyo ni:-

1.      YESU KRISTO – Mtume Mkuu aliyekuwako na aliyeko. (Ebr.3:1, Yoh.3:16, 20-21; Yoh. 4:34, 5:19, 30;  6:38; 8:28 ,29, 42;  12: 44 - 45)

2.      Mitume Kumi na wawili wa Mwana Kondoo (Ufu.21:14, Mt.19:28)

Hawa walichagulia na Yesu Kristo mwenyewe baada ya mkesha wa usiku kucha wa maombi mazito. Hawa wana nafasi maalumu mbinguni na milele, majina yao yameandikwa katika misingi kumi na mbili ya mji Mtakatifu – Yerusalemu.

Ni alama ya mwanzo wa kizazi kipya, na mwisho wa zama za unabii.

Katika agano jipya ni Mitume waliohusika na uandishi wa maandiko Matakatifu

Katika agano la kale ni Manabii waliohusika na uandishi wa maandiko matakatifu.

3.      Mitume waliotokea baada ya kupaa kwa Bwana  (Efe.4:10-11)

Mitume hawa watatenda kazi hadi kanisa liufikie umoja wa imani na kumjua Mwana wa Mungu. (Efe.4:13)

Ni wamuhimu sana katika mwili wa Kristo. Wasipokuwepo kanisa litaumia kutokana na kukosa uongozi wa maeneo mengi muhimu. (1Kor 12: 26-28)

Mifano Ya Mitume Hawa Katika Agano Jipya.

i. Androniko. Rum.16:7

ii. Yunia. Rum.16:7

iii. Tito. 2Kor.8:23

iv. Barnaba. Mdo.14:14

v. Yakobo. Gal:1:19

vi. Epafrodito. Fil.2:25

vii. Timotheo. 1The.1:1; 2:6

viii. Silvano. 1The.1:1; 2:6

ix. Apolo. 1Kor 4:6, 9.

4.      Wale Wengine Sabini (Wenye Huduma ya/ Ifananayo Na Utume)

Siyo lazima waitwe Mitume, bali huitenda / huitimiza huduma ya Kiutume.

Mfano; wale wengine sabini ambao Bwana Yesu aliwatuma (Luk.10:1-17)

Leo Je Mitume Wanahitajika?

Watu wengi leo hii katika kanisa hawaamini kwamba wapo mitume kwa nyakati hizi (au hata Manabii) Wanazikubali karama nyingine kama ya uinjilisti, uchungaji, na ualimu; sababu eti mara kanisa lilipoanzishwa katika karnee ya kwanza, hatuhitaji tena mitume na manabii, lakini je, mawazo haya ni sahihi kulingana na maandiko? (Efe.4:11-13).

Hapa biblia imeweka wazi kwamba karama za huduma tano ni za kutenda kazi “hata sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;” Yaani, kanisa liufikie;

1. Umoja wa imani

2. umoja wa maarifa ya kumjua sana Mwana wa Mungu

3. Cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo.

Kwa kulipima kanisa leo hii, bado hatujafikia maeneo haya yote, kwa hiyo kanisa linahitani karama ya huduma zote tano; ikiwemo ya huduma ya mitume.

Lakini je, leo hii wapo Mitume katika kanisa ?

BWANA Yesu Kristo bado leo hii anawatuma aliowaita na kuwapa agizo katika nguvu za Roho Mtakatifu na mamlaka, ili wafunge na kufungua, wahubiri injili, waponye wagonjwa na kufufua wafu, katika nguvu za Kristo mfufuka; kuwafikia walio gizani wangojeao kuiona nuru kuu ya Kristo YESU! Kumbuka! Jina “Mtume” Siyo la lazima, kwa sababu uthibitisho wa huduma ya kitume unaonekana katika tunda lizaliwalo kwa kazi ya Kiutume. (1Kor.9:1,2).

Sehemu Muhimu Ya Mafunzo Ya Mtume

1. Wito dhahiri katika huduma hii.

2. Kufunzwa vizuri maandiko.

3. Kuandaliwa muda wa miaka kadhaa.

4. Kujifunza chini ya huduma ya mitume wengine.

5. Kutumiwa na Mungu kati ya huduma nyingine zilizopo katika huduma tano zilizobaki.
6. Hatatumwa hadi maandalizi yake yamekamilika.

7. Kanisa linalompeleka, litamtambua na kumuwekea mikono kabla ya kwenda.


Sifa Za Mtume

Viwango/sifa za wazee zinatumika kwa viongozi wote katika ngazi za juu za mamlaka ya Kimungu na kwa mtume pia. (1Tim.3:7, Tit.1:5-9)
Licha ya viwango hivi, zipo sifa maalumu au tabia maalumu ambazo kila mtume anapaswa kuwa nazo, ambazo ni:-

1. Moyo wa Mzazi. (Kor.4:15, Fil.2:22, Efe.6:4, 1The.2:6-8,11)

2. Mwenye Saburi (2Kor.12:12)

3. Mwaminifu (1Kor. 13:)

4. Asiwe Mwenye Kujitukuza (1kor.4:9; 2kor.10:8, 1the.2:6)

5. Mwenye Moyo Wa Kutumikia, Sio Kutumikiwa. (Efe.3:7; Fil.1:11; 1kor.4:9, 2kor.10:8; 1the.2:6)

6. Awe Tayari Kuteseka (Mdo.20:17-24; 1kor.4:7-12; 11:18-30)

Huduma Ya Mtume Kazi za mtume ni kama ifuatavyo:-

1. Kuanzisha Makanisa na kuyaweka katika msingi sahihi. (1Kor.3:9-14; 9:12; 11:34; Efe.2:2-4; Rum.1:11; Kol.2:5-7)

2. Kutoa mafundisho na maandiko sahihi. (Mdo.2:42; 15:1-31)

3. Huduma ya matendo ya miujiza. (Rum.15:18, 19; 2Kor.12:12)

4. Kuliadibisha kanisa pale inaphitajika. (Mdo.5:1-11, 1Kor. 5:)

5. Kuweka uongozi katika kanisa jipya. (Mdo.6:1-6; 14:23; Tito.1:5)

6. Kuwafundisha na kuwafunza watendakazi wapya. (2Tim.2:2; Mdo.16:1-4; Fil.2:19-20; Kol.4:7-12)

7. Maangalizi ya makanisa aliyo yaanzisha. (2Kor.11:28)

8. Kutenda kazi na wazee wa kanisa, katika kuweka watendakazi wapya. (Rum.1:11; 1Tim.1:18; 4:14; 2Tim.1:6) – Kufunga na kuomba, Kuwekea mikono.
9. Kuwa mfano wa kama mzazi (baba au mama) katika familia ya Mungu. (1Kor.4:15; 1Kor.16:12, 1Pet.5:2)

10. Kuhusisha karama za huduma nyingine nne.

Mtume anatakiwa kuwa:-

Mwinjilisti- Ili kuwafanya waamini wapya.

Mwalimu- Ili kufundisha/kuelekeza katika mafundisho ya kweli.

Nabii - Ili kuleta mwelekeo na masahihisho kwa nguvu na mamlaka ya kimungu.

Mchungaji - Ili kuangalia kazi ya watendakazi wapya na makanisa. Huduma ya mtume ni ya pekee na ni mbali na huduma nyingine nne zilivyo; Mfano:-
Ni kama mkono wa binadamu, wenye vidole vine na dole gumba; Mtume ni kama dole gumba, ambalo huvigusa kirahisi vidole vingine vyote vinne, ila sio rahisi kwa kidole kingine chochote kuvigusa vidole vingine vinne, isipokuwa huweza kugusa dole gumba tu; -hiyo ina maana kuwa waamini wote wamepewa agizo kuu, umisheni!

Wito wa Mtume.  Mtume huitwa na Mungu. Ni Mungu aamuaye wapi, lini, na ni jinsi gani mtume atahudumu. Kwa ajili hiyo, mtu hatakiwi kirahisi rahisi tu kujiita mwenyewe kwamba yeye ni mtume (au nabii, muinjilisti, mchungaji, au mwalimu) WITO WA MTUME UTAJULIKANAJE? Nani atamtambua na kuithibitisha huduma yake? Njia za kufahamika na kutambulika.

1. Kujifahamu na kuwa na hakika kwa habari ya wito wake.

2. Viongozi wa kanisani kwake watamtambua kwa kazi zake.

3. Kazi zake zitamjulisha.

4. Watu wa kanisa la nyumbani/mahali nao watamtambua. Hii haimaanishi kwamba atajulikana au kupokelewa kama mtume na kanisa kiulimwengu. (1Kor.9:1-3)

2. Karama Ya Huduma Ya Nabii.

Nabii: Kiebrania = Nabi; Msemaji wa Mwingine, Mjumbe; Hozeh, Roeh = Kuona, Mwonaji. Mjumbe, Mtu Wa Mungu. UNABII Ni Ujumbe Wa Nabii. Maono, Mzigo, Utabiri Au Neno La BWANA. Kazi Za Nabii

1. Kusema Ujumbe toka kwa Mungu. (Ebr.1:1)

2. Utabiri wenye kufunua mawazo ya Mungu, kwa

a. Utabiri wa matukio yajayo, ambayo Mungu tu huyajua (Mdo.21:10-14)

b. Kuweka wazi mawazo, nia, na makusudio ya moyo wa mwanadamu (Mdo.5:3)

Yote ni kwa uongozi wa Roho Mtakatifu na sawa na unabii wa kibiblia.
Mara nyingine mahubiri huweza kuwa ya kiunabii pale ukweli ambao haukufikiriwa kwanza au utendaji unaletwa mara na Roho Mtakatifu kupitia chombo kiteule kama vile Mchungaji, Mwalimu, au mzee ambaye hana karama ya huduma ya Nabii. Nabii atauweka wazi na huutangaza moyo au nia ya Mungu kwa watu na atafunua moyo na mawazo ya watu mbele za Mungu wakati anapohudumu.

Viwango Vya (Aina Za) Unabii.

1. Unabii Wa Kimaandiko (2petr. 1:19-20) Ni unabii wa halli ya juu sana.
Unatolewa kwa uvuvio wa Mungu (2Tim.3:16) Hauna makosa Una mamlaka kamili / ya mwisho. Hautolewi tena siku hizi za leo (Ufu.22:18-19). Biblia ni kamili ni kiwango cha kupimia aina nyingine zote za unabii.

2. Huduma/Karama ya Unabii (1kor.2:10) Ni mojawapo kati ya karama tisa zitolewazo na Roho Mtakatifu. Mwamini yeyote huweza kutumiwa wakati fulani (Mdo.2:18)
Ni kwa ajili ya kuujenga, kuuhamasisha, na kuufariji mwili wa Kristo. (1Kor.14:3)
Atumiwaye kwa karama hii, haina maana kwamba yeye ni Nabii! (Hes: 11:22, 1Kor 14:24,31)

3. Karama Ya Huduma Ya Nabii Inahusiana na wito wa mtu.

Ni karama ya huduma itolewayo na BWANA YESU kwa aliyeitwa kwenye wito wa huduma ya kiuongozi katika kanisa. Kazi zake ni;

o Kuthibitisha

o Kuongoza / kuelekeza

o Kukemea

o Kuhukumu / kuamua

o Kuadibisha / kurekebisha

o Kuonya

o Ufunuo.

Asili Ya Huduma Ya Kiunabii. Mungu mara zote aliiweka sauti ya kiunabii ulimwenguni. Alichagua kusema kupitia viongozi wa kimungu hata kabla ya huduma ya nabii kutolewa.

o Habili (Luk.11:50-51) o Henoko (Yud.14) o Nuhu (Ebr.11:7, 2Petr.2:5)
o Abramu (Mwa.20:7) o Isaka (Zab. 105:9-15) o Yusufu (Mwa.50:24) o Musa (Kum.34:10) o Miriamu (Kut.7:10) o Haruni (Kut.7:1) o Debora(Amu.7:1)
Mungu alimpa Musa mwongozo wa kuwapima Manabii wote watakao tokea baadaye. Hes.12:6 Kum.18:15-22 Isa.8:19-20 Luk.16:29. Huduma maalumu ya nabii ilitolewa kwanza kwa Samweli (Mdo.3:24-25, 13:20, Ebr. 11:32)
Samweli alianzisha pia shule ya manabii. Alikuwa ni mwamuzi wa mwisho na wa kwanza kwa wale walioitwa kwa ajili ya Karama ya Huduma ya Nabii. (2Fal.2:35) Aliuweka mpangilio mpya wa kiunabii kwa watu. Walifundishwa katika neon Walikuwa makini sana kwa sauti ya Roho Mtakatifu Walimwabudu Mungu katika Roho na kweli Kila nabii alikuwa nasehemu katika urithi wa kiunabii Katika kila mfalme wa Israeli, nabii aliinuliwa ili kumweka katika njia sahihi. Miaka 400 K.K. sauti ya unabii ilikuwa kimya. Kisha ikaanza kusikika tena kwa kinywa cha Yohana Mbatizaji. Kipindi cha Agano Jipya walikuwepo manabii katika Matendo ya Mitume, kama ifuatavyo:-

MANABII WA AGANO JIPYA i. Yuda na sila (Mdo.15:32) ii. Agabo (Mdo.22:10-13) iii. Anania (Mdo.22-15) iv.Katika Antiokia (Mdo.13:1) v. Katika Tiro (Mdo.21:3-4) vi. Katika Yerusalemu (Mdo.11:27) vii. Katika Korintho (1Kor.14:29).

Mungu aliihuisha tena huduma iliyonyamaza kwa muda wa kipindi kirefu. Yesu Kristo – Nabii Ambaye Ni Kielelezo. Aliitwa nabii wa Mungu (Kum.18:15, Mdo.3:22). Watu wegi walimwona kuwa ni nabii. (Yoh.4:19; 16:14; 7:40; 9:17; Ebr. 1:1-2) Alisema yale tu aliyoyasikia kwa Mungu na aliyoyaona toka kwa Mungu alitoa unabii wa mambo yajayo Ni nabii mkuu. Kazi ya Huduma Ya Nabii

1. Huduma ya nabii huwa tofauti kati ya nabii na nabii, hazifanani kabisa.

a. Majina huonyesha hilo pia. i. Waonaji (1Sam.9:9) ii. Wajumbe (2Nya.36:16) iii. Watu wa Mungu (2Fal.12:22) iv. Watumishi wa Mungu (Amo.3:7, Zeka1:6)
b. Walipokea mafunuo yao kwa njia tofauti. i. Kwa kuona vitu katika Roho. (Mfano: - Ezikieli, Danieli na Zekaria). ii. Kwa njia ya ndoto / njozi. Kupatwa na hali ya usingizi, au kuhamishwa- kama vile roho kuondolewa katika mwili, kisha kuona vitu katika ulimwenug wa kiroho.(Mfano:-Daniel, Paulo, Yohana)
iii. Kwa kusikia sauti. Kusikia vitu katika roho. (Mfano: - Mika, Isaya, na wengineo)

c. Waliwapa watu ujumbe wao kwa njia tofauti pia. i. Kwa kusema (Isa.21:6)
ii. Kuandika (Yer.30:2) iii. Kwa mifano ya kuigiza au hadithi za kweli. (Eze.4:1-3; Mdo. 21:11) Hosea na Yoeli walitumia mifano na hadithi.

Huduma Ya Nabii Katika Agano Jipya Itahusisha 1) Ufunuo kwa: -
a) Mtizamo wa ndani wa kimungu katika neon au nia ya Mungu.
b) Ulitumiwa na mituma na manabii katika kuandika Agano jipya (Efe.2:20, 3:4-5.
c) Mtizamo maalumu wa ndani katika maisha ya watu(Mdo.5:1-11; 1Kor.14:25)
2) Mtizamo maalumu wa ndani kwa matukio yajayo (Mdo.11:27-28, 21:10-14) Nabii hawatawali viongozi au kanisa bali hutoa mwelekezo/mwongozo tu!
3) Kuhamasisha / kuchochea / kutia moyo. (Ezr. 5:1-2; 6:14; 1Kor.14:3-4; Efe.4:11-12)
4) Kuonya, kutahadharisha (Mdo.11:27-30; 21:8-11 –Ili wajiandae kwa busara kwa yale yajayo.

5) Maono kwa watu wa Mungu (Mit.29:18; Amo.3:7; Efe.3:5) –ili kutoa mwelekeo.

6) Kuanzisha makanisa mapya. (Efe.2:20; 3:5; Mdo.15:32, 41; 13:1-3)
7) Kuhudumu na manabii wengine (na mitume) kama timu au kikundi. (Mith.11:14, Mdo.11:14, Mdo.11:27-30, 1Kor. 14:29) - Ili kuleta uwiano na kuepushwa katika makosa ya kibidamu. Maonyo Kuhusu Huduma Ya Nabii

1) Maonyo ya Mungu kwa watu wake kuhusu ~ a) Kuipokea huduma ya nabii (Mt.10:41) i) Kutowakataa manabii – Mt.13:57, Mk.6:4 1The.5:20)

ii) Kanisa halitakua itakiwavyo kama manabii watakataliwa (Luk.11:48-51). b) Kujihadhari na manabii wa uongo (Yer.5:30, 31; 14:13-18; 23:9-40; Eze.13:1-23, Mt.7:15, 24:11, 24) Kuwapima kwa kupitia

(1) Neno la Mungu (2) Roho Mtakatifu. (3) Viongozi wa kiroho. (Isa.8:20, 1The.5:20-21, 1Yoh.4:1)

2) Maonyo ya Mungu kwa manabii wake. i) Wawe na kiasi (1Kor.14:32)
ii) Waruhusu huduma yao kupimwa. (1Kor.14:29) – Hakuna asiyekosea.

Njia Za Kuipima Karama Ya Huduma Ya Nabii. (1yoh.4:1)

a) Unabii unakubaliana na neno la Mungu? (Isa. 8:20).

b) Umetolewa kwa roho njema? (1Kor.13:2) c) Maneno ya Unabii yametimia? (Yer.23:13 – 16)

d) Ushuhuda wa Roho Mtakatifu unaendana na unabii? (2Petr.1:21)

e) Viongozi wa kiroro wengine wanaukubali? (2Kor.13:1)

f) Maneno ya unabii yanawaongoza watu kwa BWANA au mbali naye. (Kumb.13:1-4).

3. Karama Ya Huduma Ya Mwinjilisti.

(Mshuhudiaji/Mhubiri)
MAANA
Evanggelizo   = kuhubiri, kutangaza, kutamka habari njema - kushuhudia.
Evanggelion = Injili au habari njema na ujumbe wa furaha.
Evanggelistes = Mhubiri au mjumbe wa habari njema.

KRISTO YESU – KIELELEZO CHA MWINJILISTI

Luk. 4:43, 4:18-19, Isa.61:1-2, Agizo alilotoa katika Mk.16:15

Huduma Ya Mwinjilisti / Mshuhudiaji / Mhubiri

Katika Matendo ya Mitume sura ya .21:8, kuna Mwinjilisti wa kanisa la kwanza aliyekuwa akiitwa Filipo. Huyo alikuwa na huduma ya Uinjilisti.

 Mambo manne ya kujifunza kutoka kwa Filipo kuhusu uinjilisti;-

1.      Maandalizi Ya Mwinjilisti (Mdo.6:1-6)

a. Hutoka katika kanisa la mahali pamoja

b. Mtu wa tabia njema na mwenendo mzuri kiroho

c. Aliyejazwa Roho Mtakatifu na hekima. 

d. Aliye na moyo wa kitumishi wa upendo

e. Aliye jithibitisha kwanza kuwa ni shemasi

f. Aliye jinyenyekesha katika mamlaka ya kimungu kupitia uongozi wa kanisa la mahali pamoja.

g. Aliyeungojea wakati wa Mungu. (Mdo.8:1-5)

 

2.      Huduma ya Hadharani (Pamoja) Ya Mwijilisti Filipo ni mfano:(Mdo.8:5-25)

a. Katika mahubiri yake

i. Kristo Yesu ndiye kiini. (Mdo. 8:5-12) kwa sababu ndiye asili ya Injili

ii. Kuliambatana na ishara na maajabu ya Mungu. (Mdo.8:6-7)

b. Aliwabatiza katika maji mengi waamini wapya kama ishara ya imani (Mdo.8:12)

c. Aliwatuma kwa Petro na Yohana aliyewaongoza katika Ubatizo wa Roho Mtakatifu.

d.Waamini wapya waliwekwa katika kanisa la mahali pamoja (Mdo.9:31)
e. Hakwenda tu kuhubiri bali mpaka pale BWANA alipompa maelekezo. (Mdo.8:26), aliitii sauti ya Mungu.

f. Alikuwa na “uinjilisti wenye shabaha/malengo” – yaani, wenye makusudio ya kuwapata waamini wapya. (Mdo.8:14-17)

 

3.      Huduma Ya Binafsi (Ya Kumhubiria Mtu Mmoja Mmoja – Isiyo Ya Hadharani) Mdo.8:26-40) Inahitaji:-

a. Kuwa makini kuisikiliza sauti ya Roho Mtakatifu na kutii.(Mdo. 8:26 - 40)

b. Kuwa na ufahamu mzuri wa neno la Mungu. (Mdo. 8:35)

c. Kuwa na uwezo wa kuielezea vizuri njia ya Mungu ya wokovu kupitia Kristo Yesu. (Mdo. 8:35)

d. Kuhudumu kwa yule ambaye moyo wake uliandaliwa tayari na Mungu. (Mdo. 8:30)

e. Kuongoza kumkiri Yesu Kristo kama BWANA na Mwokozi (sala ya toba) yaani kutoa nafasi ya uamuzi wa mtu kumpokea Mwokozi Yesu. (Mdo. 8:37)

f. Kutilia muhuri uamuzi wa waamini wapya kwa Kristo kwa ubatizo wa maji mengi. (Mdo. 8:38)

 

4.      Wajibu Wa Mwinjilisti Katika Mwili Wa Kristo. (Mdo.4:11-13)
a. Kusafiri na kuhubiri injili sehemu ambako hawajasikia habari za wokovu.

b. Kuwafundisha na kuwazoeza wengine katika kanisa la mahali jinsi ya kufanya uinjilisti (Kushuhudia) kwa waliopotea.

4. Karama Ya Huduma Ya Mchungaji

Waamini huitwa kundi la kondoo wa Mungu. (Isa.40:11, Yer.13:17, Mt. 26:31, Yoh.21:15, 1Petr.5:2). 

Kondoo wanazo tabia nyingi zinazotukumbusha kwa habari ya wakristo wapya/waongofu wapya katika kujifunza kukua katika BWANA.

Tabia Za Kondoo.

1. Wanamtegemea kabisa mchungaji wao. (Mwa. 4:2, 1Sam.17:20-28)

a.      Wanahitaji

i. Kupelekwa malishoni

ii. Kupumzishwa wachokapo

iii. Kuponywa majeraha pindi wapatapo majeraha.

2. Wanautambuzi hafifu sana kuhusu mwelekeo. (Zab.119:176, Isa.53:6, Yer. 50:6, Eze. 34:12)

a.      Wakiachwa pekee, hutangatanga na kupotea njia. 

b.      Hawawezi hata kurudi nyumbani peke yao.

3. Wanao uwezo mdogo sana wa kujilinda wenyewe. (Mt.10:16, Hes.32:24)

a.      Hawana hata kucha kali au meno

b.      Hawawezi kukimbia haraka sana

c.      Wakiachwa pekee ni rahisi kuvamiwa na wanyama wa mwituni. Math10:16

4. Wanao uwezo wa kumsikia na kumfuata mchungaji wao – Kondoo husikia sauti                                     Ya mchungaji – Yoh 10:3 – 10

5. Wanatoa - maziwa, sufu, na nyama.

Maana Ya Mchungaji

Poimen = aangaliaye, atunzaye, aongozaye, na alilishaye kundi.
Poimaino = kuangalia, kutunza, kuongoza, na kulilisha kundi.

Uchungaji.

1. Uongozi.

a. Kujiangalia Wenyewe - kuwa na uweozo wa kujilisha kupitia Roho Mtakatifu

b. Kuliangalia Kundi

c. Kufanywa Na Roho Mtakatifu

d. Kuangalia

e. Kuliona Kanisa Ni Mali Ya Mungu

2. Huduma Ya Mchungaji

a. Kulitunza kundi, kulilisha, kulinywesha, kulilinda kundi la kondoo

b. Kujitoa mwenyewe kwa huduma ya unyenyekevu, kwa ajili ya hali njema ya kundi – kuwa tayari hata kufa! “ Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo” (Yoh. 10:11-15, 21:15 – 17, Ufu. 7:17)

c. Mchungaji aongozwaye na Roho Mtakatifu ni kiongozi – mtumishi

d. Huduma ya mchungaji ni kusaidia kuwaongoza watu kwenye uhusiano wa kiundani na BWANA/ MUNGU; wala sio:-

i. Kuwatawala

ii. Kuchukua nafasi ya uhusiano wa mwamini na Mungu; Ndio maana ya kupasuka kwa pazia la hekalu (Mt.27:51) Hakuhitajiki watu wa Mungu kuwakilishwa na ukuhani wa kibinadamu, Waamini wote waweza kumwendea Mungu moja kwa moja.

3. Kristo Yesu – Kielelezo Cha Mchungaji.

a. Kanisa ni watu wanaotawaliwa na Mungu – wana uongozi wa Kimungu (theocracy)

b. Mungu ni Mchungaji (Mwa.49:24, Eze 32:12-14) kwa Israeli.

i. Huwaongoza (Zab.23:3)

ii. Huwalisha (Yer.50:19)

iii. Huwaongoza na kuwanywesha (Zab.23:2, Isa.40:11)

iv. Huwalinda (Zab.23:2, Isa. 40:11)

v. Huwaita na kuwakusanya (Isa. 56:8, Zek. 10:8)

vi. Huwabeba wanakondoo kifuani mwake (Isa. 40:11)

Vii.Huwaongoza kwa upole wale wenye watoto (Isa.40:11)

c. Yesu Kristo aliivaa sura ya Mungu. Ni Mchungaji Mkuu (1Petr.5:4)

i. Mfano wa moyo wa kichungaji.

ii. Wachungaji watendaji chini ya Mchungaji Mkuu, Yesu, wajifunze kwa uangalifu moyo na msukumo wake, ili wafanane naye.

iii. Kila mchungaji awe na moyo wa kichungaji wa Yesu Kristo. Aliwapenda na kuwahurumia watu wa Mungu. (Mk.6:34) Alimthamini sana kila kondoo. (Luk. 15:4). Alikuwa tayari kuutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo (Yoh.10:11,15)

4. Sifa za huduma ya Kichungaji.

a. Aweze kuongoza kondoo (Yoh.10:4)

i. Awe na uhusiano na kutembea na Mungu binafsi kabla ya kuwaongoza wengine katika njia za Mungu.

ii. Akitaka watu wawe waombaji, watoaji, wasomaji wa neno, na watembeleaji watu, lazima awe mfano.

iii. Aishi maisha ambayo kondoo watayafuata. (1Kor.11:1, Ebr. 13:7, 1Petr.5:23)

b. Aweze kulilisha kundi. (Yer.3:15,23:4, Eze.34:1-3, Mdo. 20:28, 1Petr.5:2-3)

i. Awe kwanza ndani ya neno na neno ndani yake.

ii. Inahitaji maombi, kusoma, kufikiri, na kuwa mtendaji wa neno. (Yer. 10: 2, Mdo. 6:4)

c. Aweze Kuhubiri na kufundisha katika urahisi na uwazi ili kila mtu aelewe.

Kualika wahubiri, semina, mikutano ya injili, …

d. Awe tayari kuutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. (Yoh.10:15, 3:16, Ufu. 12:11)

i. Kujitoa kwa ajili ya watu wa Mungu, kwa: Kuumimina uhai wake na nguvu (kufunga na kuomba)

ii. Kuwatunza kondoo nyakati za uhitaji. (Eze. 34:4, Yoh. 10:13).

iii. Kukaa na kondoo nyakati za taabu. (Yoh. 10:12) Kutembelea nyumba za kondoo. (Zek.10:2,3)

iv. Kukesha kwa ajili ya usalama wa kondoo (Ebr.13:7)

 

5. Huduma Ya Mchungaji/ Kazi Za Mchungaji

1. Kuwatafuta Kondoo waliopotea. (Luk.15:4)

2. Kukesha kwa ajili ya mambo yatakayolidhuru kundi;-

a. Mbwa mwitu wakali

b. Waalimu wa uongo.

3. Kuwajali wahitaji wa: - (Yoh. 10:11-13)

a. Kiroho

b. Kimwili

i. Kifamilia, shule, na maeneo mbalimbali ya maisha.

ii. Faraja na ushauri kwa wagonjwa, wafao, viwete, masikini, wajane, yatima, na wenye kuumia.

4. Kuwarekebisha waliokosea (Zab. 23:4)

a. Fimbo ya mchungaji hutumika kuwafikia na kuwaokoa kondoo waliopotea.
b. Gongo hutumika kuwalinda wakiwa hatarini na pia kuwarekebisha wapoteao na waasi wasiosikia.

Maonyo Kwa Wachungaji

1. Asipuuzie au kutojali kukua kwake binafsi kiroho. (Yer.2:8, 1Tim. 4:15,16)
a. Kuutumia muda mwingi wa kuwa na mchungaji Mkuu.

b. Wanahitaji ulinzi kwani yeye ni lengo la kwanza la shetani. (Zek.13:7, Mat 26:31)

2. Asifanye kazi hii kwa faida yake binafsi.  (1Tim. 3:3, 1Petr. 5:) sura yote, Yoh 10:1-13

i. Mwivi

ii. Mnyang’anyi

iii. Mtu wa mshahara.

3. Asitafute nguvu za kiulimwengu. (Eze. 34:4, Luk. 22:24-27, 1Pet.5:3)

i. Kama vile

1. Siasa 2. Uongozi /utawala wa duniani

4. Asiwaendeshe kondoo (Mwa.33:13). Awe mvumilivu kwa kondoo, asije akawaacha wengine nyuma.

5. Adumishe familia ya kibiblia (Efe.5:25)

a. Mambo ambayo Mungu ameyaweka ili mtu ayape kipaumbele.-ayajali, kwanza ni:-

i. Uhusiano wa mtu na Mungu. (Yoh.15:5)

ii. Wajibu wake katika familia ya:

1. Nyumbani. 2. Watu wa Mungu –Kanisani. Efe.5:25, 33; Tito 2:4; 1Tim 3:5; 5:8)

iii. Kwa wengine.

Hukumu Kwa Wachungaji Wasio Waaminifu.

1.       Kunyang’anywa kondoo na kupewa wachungaji wale walio waaminifu. Waamini kuhama makanisani (Yer.10:21; 23:1-4)
2. Kuwa chini ya mkono wa Mungu wa hukumu nzito (Yer.10:10 13;22:22,23:1-5; 25:34-38; 50:6-7; Zek. 10:3;11:17; Mdo.20:28-38)

 

5.      Karama Ya Huduma Ya Mwalimu (Mt. 28:19 – 20)

Ni muhimu katika uanzishwaji wa kanisa.

Maana ya Mwalimu ;-

Didasko = kufundisha au kuelekeza, Ni njia ya kuelezea kitu.

Mwanzo Wa Walimu Katika Biblia;

1. Wazazi

2. Musa

3. Waandishi.

Kristo Yesu – Kielelezo Cha Mwalimu (Yoh. 3:2, 13:13)
Alifundisha kwa nguvu na mamlaka na upako wa Roho Mtakatifu. (Mt.7:28 29) Maneno yake yalihusu sana Baba yake na kazi za Roho Mtakatifu. Hii ilikuwa ni ufunguo wa huduma yake, pia kwa yeyote leo mwenye huduma ya Ualimu, atakaye kufanikiwa katika kazi ya ualimu wa neno la Mungu.

Viwango Vya Walimu

1. Kila Mwamini anatakiwa kuwafundisha wengine kuhusu maisha ya kikristo. (Mt.28:20, Kol. 3:16), hii haina maana kwamba kila mwamini ni mwalimu katika kanisa bali wapo waliopewa huduma hii kwa Neema.

2. Kila Mzazi Na Kila Mzee anatakiwa aweze kuwaelekeza wengine katika njia ya Mungu. (1Tim 3:2)

 Karama Ya Huduma Ya Ualimu Katika Kanisa.

 a. Ni mojawapo ya karama za huduma tano; itendayo kazi katika kanisa (Efe.4:11, 1Kor. 12:28-29)

b. Paulo inaonekana alikuwa Mwalimu kabla ya kuwa Mtume. (Mdo 11:26; 2Tim1:11).

Wakati ambao hakuwa katika Huduma ya Kitume, alirudi na kuwa tena Mwalimu kanisani. (Mdo.15:35)

c. Kulikuwepo na walimu wengine Antiokia. (Mdo13:1)

d. Waliiona kuwa ni huduma muhimu na waliijali sana katika kanisa (Yak.3:1)

Viwango Au Aina Za Ufundishaji (Kuhubiri Au Kusema Neno La Mungu) (1kor.14:6). Kufundisha Kwa

a. Mafunuo (Revelations)

b. Ujuzi / maarifa (Knowledge)

c. Kifuniko cha Roho / cha Unabii

d. Mafundisho (Doctrine)

Maelezo Maalumu Kuhusu Karama Ya Huduma Ya Mwalimu.

1. Upo uhusiano wa karibu sana kati ya huduma ya mwalimu na huduma ya mchungaji.

2. Huingiliana, japo kuwa si huduma moja.

3. Huduma ya mwalimu na ya mchungaji zinategemeana.

4. Mwalimu ashirikiane na mchungaji au Wazee wa kanisa katika kazi ya kuwaadibisha waamini.

5. Mchungaji awatie moyo wale wenye huduma ya Ualimu.

6. Kama nabii, Mwalimu naye anahitaji upako wa Roho Mtakatifu, lakini nabii huendeshwa na Roho Mtakatifu katika uvuvio zaidi au hali ya kutojiandaa (papo kwa papo).

7. Mwalimu mwenye upako hutenda kazi katika njia ya kipimo zaidi kwa udhahiri katika kuangazia kweli za neno la Mungu kwa namna nyepesi ya maelekezo na Ufahamu.

Mambo muhimu katika Huduma Ya Mwalimu.

Maeneo muhimu kuhusu huduma ya kufundisha.

Mwalimu anatakiwa awe na yafuatayo:-

1. Asiache kujifunza na kujiandaa. Yapo mengi ya kujifunza katika shule ya Roho Mtakatifu. (1Kor.2:13)

2. Alifahamu Neno la Mugu. (Mk.12:24). Hawezi kufundisha asicho kifahamu au asichowahi kukitumia katika maisha yake.

a. Aweze kuitumia kweli ya biblia katika hali za kimaisha. (Mk.9:14-29)

b. Aweze kuweka msingi imara wa waamini wapya. (Ebr.5:12)

3. Aweze kufundisha kwa mifano (Yoh.13:13-14)

a. Kwa kuishi maisha sawa na yale ayafundishayo, vinginevyo itakuwa ni unafiki. (Mt.23:1-3; Mdo1:1)

b. Ujumbe mkuu wa mwalimu ni jinsi alivyo yeye mwenyewe wala si asemavyo!

4. Afundishe kwa usahihi na kwa kueleweka. (2Tim.2:15)

a. Anabeba wajibu wa kufundisha kwa usahihi.

5. Atafute kuwaleta wengine katika kiwango cha ufahamu alionao yeye.     Mt.10:24-25; Mdo.20:20, 27)

6. Thawabu kubwa ya mwalimu ni kuona kuwa maisha ya wale awafundishao yanabadilishwa kwa neno la Mungu na kwa nguvu za Roho Mtakatifu. (Kumb.4:5, 14; 31:12-13)

a. Neno la Mungu hutenda miujiza ya nguvu sana pale linapofundishwa, linapopokelewa, na kulitii.

7. Asaidiwe na wale anowahudumia:

a. Ili aifanye huduma kwa wakati wote.

b. Inahitaji maombi, kusoma, kujiandaa, na kufundisha Neno.

c. Ni kazi iliyo ngumu, si kirahisi rahisi tu!

Maonyo Kuhusu Waalimu Wa Uongo.

Walimu hugusa mioyo na akili za watu. Hapandikiza tu kweli na habari, bali mwelekeo na tabia. Mwalimu anao uwezo wa kutengeneza umbile na kuutawala mwelekeo wa wanafunzi kwa mema sana au mabaya sana. Kwa ajili hiyo, Mungu anawaonya watu wake wajiepushe na waalimu wa uongo.

Aina Za Walimu Wa Uongo Ni kama ifuatavyo:-

1. Wafundishao yaipotoshayo kweli (ya uongo)- Yasiyopatana na mashauri mazima ya Mungu. (2Tim.4:3-4; 2Petr.2:1)

a. Yaipingayo / yaliyo kinyume na Kweli. (2Pet. 2:1; Isa.8:20)

b. Yaiongezeayo kweli / Yazidiyo kweli. (Ufu. 22:18, Mt. 5:37; 2Kor.1:17; Yak. 5:12)

c. Kuipunguza kweli (Ufu.22:19)

Sababu ya ubinafsi na tamaa za nafsi zao katika mioyo yao.

2. Wafundishao Mapokeo ya wanadamu kama neno la Mungu. (Mk.7:7)

a. Mawazo na matendo yao.

b. Mila na desturi.

Usipokee tu kila unachofundishwa na kukiamini bila kukipima kwa neno la Mungu kama ni kweli! (Mdo. 17:11) na neno la Mungu linasema tuzijaribu kila roho yaani tuzipime katika neno la Mungu ili tujue kuwa ni za kweli.

2.       Wafundishao kwa nia mbaya (1Kor.4:15) - Faida, Nguvu, cheo, (Tito 1:10-11; 2Pet.2:3).

Faida za Karama za Huduma Tano Na uhusiano na Wazee Wa Kanisa.

1. Mtume –Huhitajika ili Kuongoza.

2. Nabii – Huhitajika ili Kuonyesha mwelekeo

3. Mwinjilisti - Huhitajika ili Kukusanya au kuvuna.

4. Mchungaji – Huhitajika ili Kulinda au Kutunza.

5. Mwalimu – Huhitajika ili Kujenga msingi / kufundisha.

Mtume na Mwinjilisti – huhudumu pia mbali na kanisa la nyumbani - Huduma za kimisheni.
Nabii na mwalimu – huweza pia kusafiri, lakini wanayo kazi maalumu sana nyumbani.
Mchungaji - huhudumu kanisani, lakini aweza kwenda katika huduma za kimisheni.

Mamlaka Ya Wazee Wa Kanisa

Mandiko hayaonyeshi uhusiano wa moja kwa moja kati ya Huduma tano na wazee wa kanisa.

Zipo kweli kadhaa zinazo onyesha uhusiano wake.

1. Agano Jipya halitaji kamwe neno huduma tano. (Ila Efe.4:11; 1Kor. 1Kor.12 :)

a. Ni karama za huduma sio ofisi (ofisi ina maana watu huhusika katika kupiga kura au kuchagua na kisha kuwasimika viongozi au mawakili katika huduma fulani)

b. Ni karama za maongozi / maangalizi.

2. Zipo osisi za aina mbili tu katika Agano Jipya (Fil.1:1)

a. Wazee wa Kanisa

b. Mashemasi. (1Tim.3:1-15)

3. Maandiko Hutaja tu wazee “Kusimikwa” kwa maombi kufunga na kuwekewa mikono.

4. Wazee hushika nafasi ya wajibu na mamlaka katika kanisa. (1Tim. 5:17, Mdo. 20:17; 21:18-19; 11:30)

5. Baadhi ya Waliopo katika huduma tano huweza kusimikwa kuwa wazee wa kanisa.

a. Mchungaji ndiye Mkuu wa wazee wa kanisa- “Mzee kiongozi”.

b. Baraza la wazee wa kanisa latakiwa liwe na Mchungaji, Nabii, na Mwalimu- ili liwe na utendaji mzuri.

i. Mchungaji anatakiwa awe na;-

1. Moyo wa kichungaji

2. Maono ya kiunabii

3. Hekima ya mwalimu

c. Hata Mtume, Mwinjilisti, Nabii au Mwalimu lazima awe na kanisa la Nyumbani atokako!

TABIA ZA MASHEMASI – [1Timotheo 3:8-13.]

1) Ujazo wa Roho Mtakatifu

2) Mwenye upendo kwa kanisa

3) Kuwa na msimamo – mwenye kauri moja na ile ya Neno la Mungu, mchungaji pamoja na wazee wa kanisa.

4) Mwenye uamuzi mzuri, bila ya kigeugeu.

5) Wasio na tamaa wala choyo (kuhusu pesa na mali)

6) Wenye imani na uwezo wa kuitetea imani.

7) Wenye dhamiri safi

8) Wasiio na hatia – wenye maisha safi.

9) Wenye ndoa takatifu (mme na mke mmoja).

10) Wawezao kufundisha na kuelekeza wengine.

11) Kukubalika / kutokulaumika

12) Wenye kiasi (kujitawala) na busara

13) Wenye kufuata utaratibu (mpangilio/ratiba na kanuni)

14) Ukarimu (ukaribishaji)

15) Wenye kujua kufundisha (mwalimu)

16) Si mtu wa kujadiliana (Mbishi)

17) Mwenye kuisimamia nyumba yake vizuri – mwenye sifa nzuri nyumbani.

18) Asiwe mchanga kiroho.

19) Mwenye ushuhuda mzuri kwa wasioamini pia.

20) Mwenye kupenda kutumikia na si kutumikiwa.

KAZI ZA MASHEMASI

1) Kusimamia taratibu zote za kikanisa, kama vile

a) Usafi na upambaji wa kanisa

b) Kupanga ukaaji wa watu kanisani

c) Ulinzi wa kanisani wakati wa ibada

d) Kusimamia upishi na uugawaji wa vyakula

e) Kuwakarimu wageni - kuwapokea, kuwakaribisha, kupata taarifa zao na kuwapa maelekezo.

f) Kuwahudumia wagonjwa na wasiojiweza

g) Kuwasaidia wanaodondoka na wenye mapepo wakati wa maombezi

h) Kusimamia ratiba za kikanisa.

2) Kusimamia waamini wa mtaani kwako

a) Kusimamia ibada za nyumba kwa nyumba

b) Kuwahudumia washirika walio wajane, yatima, wagonjwa na wasiojiweza.

c) Kusaidia mawasiliano ya kikanisa wakati wa ibada na hata wakati mwingine.

d) Kufuatilia taarifa za washirika.

3) Kufundisha, kuonya, na kuelekeza na kuwatia moyo washirika.

4) Kushirikiana na kufanya kazi kwa upendo pamoja na mchungaji na wazee wa kanisa;-

a) Kusaidiana pamoja na wazee wa kanisa katika kusimamia kazi za kanisa.

b) Kutunza pesa na mali za kanisa pamoja na kumbukumbu za kanisa.

c) Kusimamia na kuhimiza utekelezaji wa maagizo ya kanisa la mahali;

d) Kusimamia na kuhimiza utekelezaji wa maagizo toka ngazi za juu.

e) Kujitoa kwa hali na mali, ili kuifanya kazi ya Mungu.

5) Kuwa mshauri wa mchungaji na wazee wa kanisa.

6) Kuliombea kanisa.

7) Kuiombea, kuihudumia, na kuitunza nyumba na familia ya mchungaji.

WAZEE WA KANISA. TABIA ZA WAZEE WA KANISA. [1Tim. 5:17, Mdo. 20:17; 21:18-19; 11:30; 1Timotheo 3:1-7]

1) Ujazo wa Roho Mtakatifu

2) Mwenye upendo kwa kanisa.

3) Kuwa na msimamo – mwenye kauri moja na ile ya Neno la Mungu, pamoja na

Mchungaji

4) Mwenye uamuzi mzuri, bila ya kigeugeu.

5) Wasio na tamaa (ya pesa)

6) Wenye imani na uwezo wa kuitetea imani.

7) Wenye dhamiri safi

8) Wasiio na hatia – wenye maisha safi.

9) Wenye ndoa takatifu (mme na mke mmoja).

10) Wawezao kufundisha na kuelekeza wengine.

11) Kukubalika / kutokulaumika

12) Wenye kiasi (kujitawala) na busara

13) Wenye kufuata utaratibu (mpangilio/ratiba na kanuni) 

14) Ukarimu (ukaribishaji)

15) Wenye kujua kufundisha (mwalimu)

16) Si mtu wa kujadiliana (Mbishi)

17) Mwenye kuisimamia nyumba yake vizuri – mwenye sifa nzuri nyumbani.

18) Asiwe mchanga kiroho.

19) Mwenye ushuhuda mzuri kwa wasioamini pia.

20) Mwenye kupenda kutumikia na si kutumikiwa.

KAZI ZA WAZEE WA KANISA

Ni watendaji wakuu wa shughuli zote za kikanisa

a) Kuliombia kanisa

b) Maangalizi ya kanisa

i) Kusimamia taratibu zote za kikanisa, kama vile;-

(1) Usafi na upambaji wa kanisa

(2) Kupanga ukaaji wa watu kanisani

(3) Ulinzi wa kanisani wakati wa ibada

(4) Kusimamia upishi na uugawaji wa vyakula

(5) Kuwakarimu wageni - kuwapokea, kuwakaribisha, kupata taarifa

zao na kuwapa maelekezo.

(6) Kuwahudumia wagonjwa na wasiojiweza

(7) Kuwasaidia wanaodondoka na wenye mapepo wakati wa

Maombezi

(8) Kusimamia ratiba za kikanisa.

ii) Kusimamia waamini wa mtaani kwako

(1) Kusimamia ibada za nyumba kwa nyumba

(2) Kuwahudumiawashirika walio wajane, yatima,

wagonjwa na wasiojiweza.

(3) Kusaidia mawasiliano ya kikanisa wakati wa ibada na

hata wakati mwingine.

(4) Kufuatilia taarifa za washirika.

(5) Kufundisha, kuonya, na kuelekeza na kuwatia moyo

washirika.
iii) Kushirikiana na kufanya kazi kwa upendo pamoja na mchungaji ambaye ndiye kiongozi katika Wazee

(1) Kuwa washauri wa mchungaji

(2) Kufundisha na kuhubiri Neno la Mungu.

(3) Kuongoza- kuelekeza kinachotakiwa kufanyika na  kuweka utaratibu wa kazi

(4) Kuwatunza washirika wasipotee

(5) Kupima na kutathimini matokeo na kiwango cha  utekelezaji

(6) Kusimamia mipango ya kanisa ili matokeo yake yawe mazuri

(7) Kuviangalia na kuvitunza vitu vyote vya kanisa

(8) Kuwa mbunifu na karibu sana na mchungaji katika kupanga mipango mbalimbali na kuangalia matokeo yake,
(9) Kusaidiana pamoja na mchungaji katika kusimamia kazi za kanisa.

(10) Kusimamia na kuhimiza utekelezaji wa maagizo ya kanisa la mahali;

(11) Kusimamia na kuhimiza utekelezaji wa maagizo toka ngazi za juu.

(12) Kujitoa kwa hali na mali, ili kuifanya kazi ya Mungu.
(13) Kuwaadibisha washirika weye mwenendo usio sahihi.

(14) Kuongoza ibada ya mazishi (kwa kibali cha mchungaji kama ikibidi)

iv) Kutunza pesa na mali za kanisa pamoja na kumbukumbu za kanisa.

2) Kuiombea, kuihudumia, na kuitunza nyumba na familia ya mchungaji.

a) Kuwa msemaji wa mahitaji, utunzaji na kuitegemeza nyumba na familia ya mchungaji - kwa kanisa.

 

 

HITIMISHO

Ni muhimu sana kwa kila mwamini aliyeokoka kutambua huduma yake aliyopea na Mungu na kuifanyia kazi kwa moyo mkuu bila ulegevu, kwani kwa kufanya hivyo tutaujenga mwili wa Kristo ambalo ndilo kanisa alilolinunua kwa damu yake ya thamini na kulitolea uhai wake. Kwani biblia inaweka wazi kuwa “amelaniwa mtu Yule aifanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu. Kila mmoja wetu baada ya kukoka Mungu ameweka huduma fulani ndani yake ili kusudi alitumikie kusudi la Mungu katika Kanisa.   

 

Mungu awabariki kwa viwango vya juu.

Mwl. Musa Festo

Contacts: mussafesto@gmail.com

+255675415262

 

 

Comments

Popular posts from this blog

JIFUNZE KUTII UPATE KUTIISHA