UMUHIMU WA KUJIJENGEA UWEZO ILI KULIBEBA
KUSUDI LA MUNGU
KATIKA MAISHA YAKO. (CAPACITY
BULDING).
NA MWL. MUSA FESTO
MAANDIKO YA MSINGI.
"Lakini,
kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu
na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele"(2Petro
3:18).
" Lakini nasema ya kuwa
mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa
yote"(Wagalatia
4:1)
MISINGI YA UUMBAJI.
Mungu alipokuwa anamuumba mwandamu
na kumleta duniani kwa ajili ya kusudi lake kuna kiwango maalumu cha
"kiutumishi"(kusudi na mapenzi makamilifu ya Mungu) ambacho Mungu
alimpangia kila mmoja ili kwa kiwango hicho mwanadamu alitumikie kusudi la
Mungu katika nyanja mbalimbali za
kielimu,kiuongozi,kisiasa,kihuduma,kifamilia,kazi.n.k.
"Maana tu kazi yake,
tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu
aliyatengeneza ili tuenende nayo"(Waefeso 2:10).
Tuone pamoja, anaposema "tutende metendo mema...... ambayo
tokea awali Mungu aliyatengeneza tuenende nayo” ...sasa anapozungumzia
tutende metendo mema. maana yake yapo mambo ambayo tunatakiwa kufanya, mahali
pa kufanya na kiwango cha kuyafanya na kuyakamilisha hayo mambo katika kiwango
ambacho Mungu alikusudia tokea awali yaani kabla ya kuumbwa kwa Misingi ya
ulimwengu.
Daudi
anasema.........
"
Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia,
Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado"(Zaburi 139:16).
Kitu gani nataka tutazame pamoja, ni
hapo anaposema hayo maneno anamaanisha kuwa siku zake zote ambazo Mungu alikuwa
amekusudia katika maisha ya Daudi yaani kazi, utumishi, mahali, kiwango cha
utumishi kilikuwa kimeratibiwa kule juu mbinguni hata kabla Daudi hajafanywa
katika mwili huu wa damu na nyama.
Bwana Yesu
pia alizungumza maneno kama aliyosema Daudi pia......
"Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la
chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu"(Waebrania 10:7).
Kitu gani nataka tuone pamoja
anaposema "katika gombo la chuo nimeandikwa”, maana yake ni kwamba Bwana
Yesu anakiri ya kwamba maisha yake yote yameratibiwa katika gombo la chuo.
Sasa kwa mifano hiyo angalao kwa
sehemu unaweza pata picha kwa sehemu ya kuwa kipo kiwango ambacho Mungu ameweka
kwa kila mmoja ili aweze kukifikia anapotembea katika kusudi na mapenzi ya
Mungu akiwa hapa duniani.
Sasa katika kulitimiza kusudi la
Mungu duniani ipo sehemu ya Mungu katika kumsaidia mwanadamu ili aweze
kulitumikia shauri la Bwana lakini ipo sehemu ya mwanadamu katika kushirikiana
na Mungu ili kuweza kufikia katika kiwango ambacho Mungu alimuwekea kabla ya
kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.
Tunapoangalia sehemu ya Mwanadamu
katika kushirikiana na Mungu ndipo tunazungumzia "umuhimu wa kujijengea uwezo
binafsi ili kuweza kuibeba ndoto ya Mungu/Kusudi la Mungu katika maisha yako).
Unapozungumzia kwa habari ya kusudi
la Mungu ni sababu ya kitu fulani kuwepo (The original intention of creation/making
something). Mungu alipokuwa anamuumba mwanadamu kwa kusudi lake kuna
vitu alimuumbia ndani yake kama vile vipaji, karama na huduma ili kwa hizo
aweze kulitumikia kusudi la Mungu.
Lakini pia kuna vitu vingine
alivifunga kwenye mazingira yanayomzunguka mwanadamu kama vile kiwango cha
elimu, aina ya masomo, mahali pa kuishi, mahali pa kufanyia kazi n.k.
Hivyo vyote Mungu amevifunga kwa
ajili ya kumsaidia mwanadamu kufika mahali ambapo Mungu anataka aweze kufika.
Sasa sehemu kubwa ya mwanadamu ili
kuweza kuyafanya hayo yote huku akishirikiana na Mungu ni kwa kujijengea uwezo
ili kuweza kutembea katika kiwango ambacho Mungu amekikusudia kwa ajili yake
kabla ya kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.
"
Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze;
ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako"
(Isaya
54:2).
Yapo mambo kadhaa ambayo nataka
tuangalie pamoja katika huo mstari angalau kwa sehemu.....
•
Anaposema.... "panua
mahali pa hema yako......”, maana yake ni kuwa kila mtu ana "hema”,
ambamo ndani ya hema kuna vitu mbalimbali kama vile viti,watu,na mambo mengine
mengine,kwa hiyo kwa maana nyingine hema ni kama kibebeo cha hayo mambo yote
yaliyomo ndani.Sasa Mungu anampa mwanadamu ndoto katika mfumo wa picha
inayojengeka ndani yake inayompa kusudi la kufanya jambo fulani.Kwa hiyo katika
hilo neno Mungu anamaanisha kuwa ongeza uwezo wako wa kuibeba ndoto ya Mungu.
•
Anaposema".....Ongeza
urefu wa kamba zako",maana yake ni kwamba kamba inaunganisha sehemu
moja na nyingine,kwa hiyo huyo mtu alikuwa anaenda kulingana na urefu wa
kamba,kamba inapoishia ndiyo mwendo wako unaishia hapo.Sasa anaposema hilo
jambo anamaanisha ya kuwa ongeza kiasi cha umbali wa ndoto uliyonayo.
•
Anaposema ".....vikaze
vigingi vya hema yako....",anamaanisha ya kuwa mhimili wa hema hiyo ni
vigingi vinavyoshikilia hilo hema (Nguzo),kwa maana rahisi hapo anamaanisha
kujenga msuli wa ndani utakaokusaidia kuibeba hiyo hema(Ndoto ya Mungu) kwa
kujenga mahusiano mazuri na mtoa ndoto,yaani Mungu,yeye anayeweza kuimarisha
misuli yako na kushiriki katika kukujengea uwezo huo kwani .... "Bwana asipoijenga nyumba Waijengao
wafanya kazi bure"(Zaburi 127:1a).
Ni nia na
makusudi kabisa ya Mungu kuona watoto wake wakijijengea uwezo binafsi kwa
kushirikiana na Mungu ili kuibeba ndoto ya Mungu.
Kwa kadri unavyozidi kujijengea
uwezo binafsi wa kuibeba ndoto ya Mungu katika maisha yako ndivyo ambavyo Mungu
atakupa hatua zaidi.
TUJIFUNZE KUTOKA KWA HAWA NDUGU
KATIKA IMANI.
Mfano
wa kwanza.
Mungu
alipokuwa anamwita Abrahamu. (Mwanzo 13:14-15).
Tunaposoma
kwa habari za Baba yetu katika imani (Abraham) Mungu alipomwita na kumwambia na
kumilikisha baraka kwa ajili yake na uzao wake alimwambia maneno
yafuatayo......
"
Bwana akamwambia Abramu, alipokwisha kutengana na Lutu,
Inua sasa macho yako, ukatazame kutoka
hapo ulipo, upande wa kaskazini, na wa kusini na wa mashariki na wa
magharibi; maana nchi hii yote uionayo,
nitakupa wewe na uzao wako hata milele"
(Mwanzo
13:14-15).
Kuna mambo nataka tuyatazame pamoja katika mistari hapo
juu...
I).Unapotaka
kujijengea uwezo katika jambo fulani ni lazima uwe na mtazamo thabiti juu ya
hilo jambo (to
have a focus) .Kwa hiyo kuna watu,marafiki na vitu vingine ambavyo
kwako ni muhimu sana lakini katika hilo jambo unalotaka kujijengea uwezo
havitakufaa ni lazima ukubali gharama ya kuviacha ili kujijengea uwezo katika
eneo sahihi.Mungu alimwambia Abram alipokuwa anamtoa Uru ya wakaldayo kuwa
awaache hata ndugu zake lakini yeye aliondoka na Rutu (Mwanzo 12:1-5,Mwanzo 11:7).Baada
ya Abramu kuachana na Rutu ndipo Mungu akazungumza naye (Your association will
determine your destination).
II).Suala
la kujijengea uwezo ni suala la maelekezo na maagizo na Ruhusa ya Mungu kwa
mwanadamu.Hakuna mwanadamu ambaye anaweza akajijengea uwezo pasipo
kumshirikisha Mungu kwa sababu yeye ndiye aliyemuumba mwanadamu kwa hiyo anajua
alimuumba kwa kazi gani kwa hiyo hata katika eneo la kujijengea uwezo ni suala
la Mungu zaidi......."inua
sasa macho yako ukatazame kutoka hapo ulipo...."
" Bwana asipoijenga nyumba Waijengao
wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha
bure"(Zaburi 127:1).
III). Japokuwa suala
la kujijengea uwezo binafsi linamhitaji Mungu zaidi kuwa kama kitovu (center)
linahitaji pia utayari wa mwanadamu katika kushirikiana na Mungu ili aweze
kujijengea uwezo katika eneo husika. Mungu alivyomwambia Abram inua sasa macho
yako ukatizame...uamuzi wa kuinua au kutokuinua...kutizama au kutokutizama
ulikuwa mikononi mwa Abram.Mungu haitaji mtu aliyekamilika hata siku moja,anamhitaji
mtu aliye tayari,ili amkamilishe katika neema yake na ukamilifu wake.....
III).Mungu alimwambia Abramu atizame pande zote mpaka pale
upeo wa macho yake utakapofikia,na ule ukubwa wa nchi auonao kulingana na upeo
wa macho yake Mungu atampa aimiliki,hii inamaanisha ya kuwa katika ile nchi ni
lazima kulikuwa na milima,mabonde ,mito na mambo Mengine mengi ambayo
yangemfanya Abram asione mbele zaidi,lakini Mungu alimwambia kitu cha ajabu
sana kuwa........maana nchi hii yote uionayo, nitakupa wewe na uzao
wako hata milele",hii inamaanisha ya kuwa
"kiwango
cha upeo wa macho yake kuona utakapoishia ndipo kiwango cha urithi wake na uzao
wake utakapoishia",sasa hapa suala la Abramu kujijengea uwezo
binafsi wa kujenga kuona zaidi ile nchi kwa kukabiliana na milima,mito,mabaonde
na mambo yanayofanana na hayo ulikuwa ni wa muhimu sana kwake.Mungu asingeweza
kumpa urithi zaidi ya pale mahali upeo wa macho yake umeishia.
Mfano
wa Pili.
Watumwa
waliopewa talanta.
Jambo la
kwanza:
Mungu anakupa kitu kulingana na uwezo ulionao.
"
Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao
mali zake. Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja
talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri". (Mathayo
25:14-15).
Kitu gani
nataka tutizame pamoja katika mstari huo ni kwamba Mungu alitoa talanta kwa
kila mmoja kulingana na uwezo alionao wa kuibeba hiyo talanta, kwa hiyo hakuna
namna Mungu anavyoweza kukupa kitu chochote kama hauna uwezo wa kukibeba kitu
hicho.
Jambo la pili: Kwa kadri unavyoongeza uwezo wa kuibeba ndoto ya Mungu
katika maisha yako ndivyo Mungu anazidi kuipanua hema yako na kukuongeza.
"Baada ya siku nyingi akaja bwana wa
watumwa wale, akafanya hesabu nao.
Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta
talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama,
talanta nyingine tano nilizopata faida.
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa
mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana
wako. Akaja na yule aliyepokea talanta
mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine
mbili nilizopata faida. Bwana wake
akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache,
nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako. Akaja na yule aliyepokea talanta moja,
akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda,
wakusanya usipotawanya; basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika
ardhi; tazama, unayo iliyo yako. Bwana
wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna
nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa
watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake. Basi,
mnyang'anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
(Mathayo
25:19-28).
Tunaposoma habari hiyo tunaona namna
ambavyo wale watumwa ambao walipewa talanta tano na mwingine mbili waliweza
kuzalisha mara mbili zaidi na hivyo wakawa wameongeza uwezo wao wa kubeba kile
kitu Mungu kawapa na kumzalia Mungu matunda, lakini yule mmoja ambaye Mungu
alimpa talanta moja kwa kadri ya uwezo alionao hakuweza kumzalia Mungu matunda
akanyanganywa ile talanta ambayo Mungu alimpa na akapewa mtu mwingine aliyekuwa
amejijengea uwezo wa ndani wa kuibeba ndoto ya Mungu.
Inawezekana kabisa kujijengea uwezo
wa kuibeba ndoto ya Mungu, haijalishi mazingira uliyonayo lakini inawezekana, hao
ndugu wote walikuwa ni watumwa ambao wamepewa talanta, sasa unaweza ukaelewa, mtumwa
muda si mali yake na siku zote hana uhuru wa kufanya kazi kama mtu aliye huru, lakini
kwa nini hao watu wanaoishi katika mazingira yanayofanana karibu kwa kila kitu
mmoja afanikiwe kuzalisha zaidi na mwingine hata akashindwa???... ukiamua
inawezekana.
" Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa
tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa"(Mathayo
25:19).
Mfano wa tatu.
Bwana Yesu alipokuwa akiwaaga wanafunzi wake. (Yohana
16:12).
Tunaposoma
habari za Bwana Yesu namna alivyokaa na wanafunzi siku zote alipokuwa akitembea
katika kulibeba kusudi la Mungu, Bwana Yesu alikuwa akijitahidi kuwajengea
"uwezo binafsi" kila mmoja, ndiyo maana alikuwa akiwasisitiza sana
kwa habari ya swala la Maombi.
Lakini alipokuwa akiondoka kuna kitu
cha ajabu sana aliwaambia......
"Hata bado nikali ninayo mengi ya
kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa"
(Yohana 16:12).
Kitu gani
Yesu kilimzuia kuzungumza na hao wanafunzi wakati anaondoka ni kwamba walikuwa
hawana uwezo wa kuyabeba hayo mambo, alikuwa anazungumza juu ya kujijengea
uwezo binafsi ili waweze kukibeba kile kitu Yesu atawaamba. Ndiyo maana Yesu
anasema kuwa anakupa kitu kulingana na uwezo ulionao kukibeba. Kwa kadri
unavyoendelea kujijengea uwezo katika eneo husika ndivyo Mungu anazidi
kuachilia maono na ndoto zake kwako.
Mfano wa nne.
Wana wa Israeli wakiwa katika nchi ya ahadi.
Tunaposoma
kwa habari za wana wa Israeli tunaona ya kuwa Mungu aliwapa nchi ya Kaanani
yenye maziwa na asali ili waimiliki.
"Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia, Tuma watu,
ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli;
katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati
yao". (Kutoka 13:1-2).
Kitu gani nataka tuone pamoja mahali
hapo, ni hayo maneno ambayo nimeyapigia mstari, Mungu aliwapa wana wa Israeli
hiyo nchi kwa sababu alijua ya kuwa wanao uwezo wa kuimiliki.
Lakini kuna kitu nataka tuone pamoja
mahali hapo, ile nchi ilikuwa inakaliwa na majitu yenye nguvu kiasi cha kwamba
hata wale wapelelezi wengine walipokwenda walijifananisha kama mapanzi. (Kutoka 13:31-33).
Japokuwa
ni Mungu aliwapa hiyo nchi kwa kujua kabisa wanao uwezo wa kuimiliki hiyo nchi,
Mungu aliwaambia kitu cha ajbu sana wana wa Israeli.
" Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi
isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua. Nitawafukuza kidogo
kidogo mbele yako, hata utakapoongezeka wewe, na kuirithi hiyo nchi"(Kutoka
23:29-30).
Kwa maneno hayo niliyoyapigia
mstari, Mungu alikuwa anamaanisha kuwa uwezo wao wa kuimiliki nchi
utakapoongezeka, ndivyo ambavyo Mungu atawafukuza maadui katika ile nchi
aliyowaahidi na kuwapa wana wa Israeli. (Capacity bulding).
Mfano wa tano.
Musa katika kuwahukumu watu (kutoka 18).
Ilikuwa ni
baada ya Mungu kuwatoa kutoka Misri na kuingia katika nchi ya ahadi ambayo
Mungu amewapa, huduma ya Musa sasa ikachanua, idadi ya watu aliokuwa
anawahudumia ikawa kubwa sana kiasi ambacho Ilimbidi Musa awe anawahukumu watu
hao kuanzia asubuhi hata jioni
(kutoka
18:13-14).
Mungu alimtumia mkwewe Musa yaani
mzee Yethro kuzungumza na Musa maagizo haya.....
"....
Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe
kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao"
(kutoka 18:19).
".......Zaidi ya hayo utajipatia
katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli,
wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu,
na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; nao wawaamue watu
hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno
dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao
watauchukua huo mzigo pamoja nawe”. (Kutoka
18:21-22).
Kitu gani nataka tujifunze mahali
hapo ni kuwa Mungu alizungumza na Musa kwa kumtumia mzee Yethro kuwa achague
watu wenye uwezo ambao kila mtu atasimsmia kundi la maelfu, mia hamsini na kumi
kulingana na uwezo alionao. Kwa hiyo hii inatujulisha kuwa Mungu anatoa kitu
kulingana na uwezo ulionao. Inawezekana ndani yako kuna ndoto ya kuwa kiongozi
katika nyanja mbalimbali za kisiasa, kiuchumi, kihuduma n.k. Ni muhimu sana
kuendele akujijengea uwezo ili uweze kuibeba hiyo ndoto.
Mfano wa sita.
Daudi alipokuwa anamkabili Goliath (1samweli 17:34-37).
Ndoto ya Mungu juu ya Daudi ilikuwa
ni kumtumia Daudi ili kumuua Goliathi. Lakini Mungu hakumkutanisha Daudi moja
kwa moja na Goliathi, nilimbidi Mungu ampitishe kwanza Daudi kwenye mazoezi
madogomadogo akiwa machungani ili "kumjengea uwezo" kabla hajakutana
na Goliath.......
Daudi akieleza namna alivyojijengea uwezo akiwa
machungani....
"Daudi akamwambia Sauli,
Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na alipokuwa akija simba,
au dubu, akamkamata mwana-kondoo wa lile kundi, mimi hutoka nikamfuata,
nikampiga, nikampokonya kinywani mwake; na akinirukia, humshika ndevu zake,
nikampiga, nikamwua, Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti
asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye
hai."(1Samweli 17:34-36).
Hapo Daudi alikuwa akitaja wasifu
wake (CV) mbele za mfalme sauli, alichokuwa anaeleza hapo ni uwezo alionao, na
kitu gani Sauli alikuwa anatafuta kwa Daudi ni "kujua uwezo alionao" wa kupambana na Goliath.
Alipokuwa
akikabiliana na Goliath alisema maneno haya...........
"Daudi akasema, Bwana aliyeniokoa na
makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu.
Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na Bwana atakuwa pamoja nawe"(1Samweli 17:37).
Mfano wa saba.
Daudi alipokuwa anapewa nafasi kuwa mfalme wa Israeli. (1Samweli
1:1-3).
Ndoto
ya Mungu kwa Daudi ilikuwa ni kumtoa Daudi katika hali ya chini sana na kumweka
kuwa mfalme wa taifa la Israeli badala ya Sauli.
" Bwana akamwambia Samweli, Hata lini
utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako
mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia
mfalme katika wanawe"(1Samweli 16:1).
"Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye
mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa
nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama"(1Samweli 16:13).
Lakini pamoja na kwamba Mungu alikuwa amemkusudia Daudi kuwa
mfalme wa Israeli yenye jumla ya kabila kumi na mbili, Mungu alimchukua Daudi
hatua kwa hatua......
Hatua ya kwanza.
(2Samweli 2:4).
"Basi watu wa Yuda wakaenda, wakamtia
Daudi mafuta huko, awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Wakamwambia Daudi
wakasema, Watu wa Yabesh-gileadi ndio waliomzika Sauli"(2Samweli 2:4).
Ndoto
ya Mungu juu ya Daudi ilikuwa ni kuwa mfalme wa taifa la Israeli lenye jumla ya
kabila kumi na mbili, lakini kwa mara ya kwanza Mungu alimpa Daudi kuwa
kiongozi wa kabila la Yuda.
Kumbuka
kuwa ndani ya Daudi Mungu alikuwa ameweka ndoto na nguvu (upako) wa kuwa mfalme
juu ya Taifa la Israeli kama tulivyokwisha kuona hapo juu. (1Samweli 16:13).
Daudi alikaa hapo akijenga uwezo wa kuibeba ndoto ya Mungu
kwa miaka saba na miezi sita....
"Huko
Hebroni alitawala miaka saba na miezi sita"(2Samweli 5:5a).
Hatua ya
pili (2Samweli 5:3).
Baada ya Daudi kuwa mwaminifu kuliongoza kabila moja (Yuda)
na kujenga uwezo wa kuibeba ndoto ya Mungu ndipo Mungu akampa taifa zima la
Israeli lenye kabila kumi na mbili..........
"
Basi wazee wote wa Israeli wakamwendea mfalme huko Hebroni, naye mfalme Daudi
akapatana nao huko Hebroni mbele za Bwana; wakamtia Daudi mafuta awe mfalme
juu ya Israeli. Daudi alikuwa amepata miaka thelathini alipoanza kutawala,
akatawala miaka arobaini. Huko Hebroni alitawala miaka saba na miezi sita; na
katika Yerusalemu alitawala miaka thelathini na tatu juu ya Israeli wote na
Yuda"(2Samweli 5:3-5).
Ilikuwa ni lazima Daudi aweze
kujijengea uwezo binafsi ili aweze kuibeba ndoto ya Mungu kuwa mfalme wa
Israeli, kumbuka baada ya kuwa mfalme wa Israeli mji wake mkuu ulikuwa ni
Yerusalemu iliyokuwa inatawaliwa na Wayebusi ambao walikuwa ni watu mashujaa, ilikuwa
ni lazima Daudi awaondoe Wayebusi ili aweze kutawala nchi hiyo, na ndiyo maana
Kabla ya kukutana na Yebusi Mungu alimpitisha kuwa Mfalme wa Yuda ili ajijengee
uwezo wa kuikabili hiyo changamoto.
"
Kisha mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu ili kupigana na Wayebusi, wenyeji
wa nchi ile; hao ndio waliomwambia Daudi, wakisema, Usipowaondoa vipofu, na
viwete, hutaingia humu kamwe; huku wakidhania ya kuwa Daudi hawezi kuingia
humo. Lakini Daudi aliipiga ngome ya
Sayuni; huu ndio mji wa Daudi"(2Samweli 5:6-7).
Mfano wa saba: Waebrania
"Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita),
mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi
mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. (13) Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la
haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. (14) Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima,
ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na
mabaya"(Waebrania 5:12-14).
MAMBO
YA MSINGI YATAKAYOKUSAIDIA KUJIJENGEA UWEZO BINAFSI ILI KULIBEBA KUSUDI LA
MUNGU KATIKA MAISHA YAKO.
i). TAFUTA KULIJUA KUSUDI LA MUNGU KATIKA
MAISHA YAKO.
Hii ni Hatua ya kwanza na ya msingi
kabisa katika kujijengea uwezo binafsi wa kuibeba ndoto ya Mungu katika maisha
yako.
•
Kusudi linakupa kujua sababu ya
kuumbwa kwako, (The reason for creation). Ulimwengu huu tunaoishi una mambo
mengi ya kila namna ambayo yanaweza kutumika kama upepo kukuyumbisha huku na
kule na hivyo ukashindwa kuwa na mwelekeo thabiti juu ya maisha yako. Kulijua
kusudi la Mungu itakusaidia kupanga mipango, kuwekeza nguvu, muda, fedha na kuweka
vipaumbele kwa kuangalia kusud, yaani unaishi maisha yanayoongozwa na kusudi "Purpose
driven life".
"Mna
hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama"(Mithali
19:21).
•
Mungu huweka Maono, ndoto na
matamanio ndani ya mtu kulingana na kusudi ambalo amemuumbia. Kusudi la Mungu
limewekwa katika namna ya picha ndani ya mtu inayoonesha kukamilisha jambo
fulani au mwisho wa jambo fulani. Mungu anaweza weka ndani yako ndani yako
ndoto ya kuwa kiongozi katika nyanja ya siasa, huduma, uimbaji.n. k Ni muhimu
sana ya kuanza kujenga uwezo katika maeneo hayo.
"
nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado;
nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote"(Isaya
46:10).
•
Ipo neema ya kukua unaposimama
katika kusudi na mpango wa Mungu.Mungu alituumba wanadamu tofauti tofauti na
aliiweka neema ya kukua kwa kila mmoja katika eneo lake. Kama wewe Mungu
alikuumbia kuwa mwalimu. itakuwa ni vigumu sana kukua katika uinjilisti, kama
alikuumbia kuwa daktari itakuwa vigumu sana kukua katika engineering.
"Lakini, kueni katika neema, na
katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata
milele"(2Wakorintho 3:18).
"Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye"
(1Wakorintho
3:7).
ii).
UHUSIANO WAKO BINAFSI NA MUNGU.
Uhusiano wako binafsi na Mungu ni
jambo la Msingi sana katika kujijengea uwezo binafsi wa kuibeba ndoto ya Mungu
katika maisha yako. Itakuwa ni vigumu sana kulijua kusudi la Mungu katika
maisha yako kama hauna mahusiano binafsi na Mungu, kumbuka kwamba Mungu
aliyekuumba anajua kuwa alikuumba kwa kazi gani, kwa hiyo ukitaka kujua kazi
yako hapa duniani ni lazima uende kwake yeye aliyekutengeneza (The
manufacturer know the purpose of the products).
Swala la mahusiano binafsi na Mungu
sio swala la kufuata mkumbo au kundi, kumbuka nimesema kuwa "mahusiano binafsi" kiasi
ambacho Mungu anazungumza na kuhusika kikamilifu katika hatua za maisha yako.
Unapozungumzia swala la kujijengea
uwezo binafsi wa kuibeba ndoto ya Mungu katika maisha yako uwe na uhakika kuwa
Mungu mwenyewe anahusika kikamilifu katika kukujengea huo uwezo kwa sababu yeye
ndiye muumba wako, anajua unatakiwa ubebe kitu gani, na anajua hicho kitu
unachotakiwa kukibeba kinahitaji nguvu kiasi gani na anajua ya kuwa unatakiwa
kwenda umbali kiasi gani na hiyo ndoto, na tena anajua ifanyike kwa ustadi
kiwango gani.
Usije ukafanya kosa la kujijengea
uwezo wa kuibeba ndoto ya Mungu katika maisha yako huku ukimwacha yeye
anayeijua ndoto yake juu yako pembeni. Kumbuka hili ya kuwa uhusiano wako na
Mungu ni wa Muhimu sana kuliko utumishi wako mbele za Mungu (Your
relationship with God is more important than your mission for God).
" Bwana asipoijenga nyumba Waijengao
wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha
bure"(Zaburi 127:1).
III). KUWA NA TAARIFA SAHIHI.
Kuwa na taarifa sahihi juu ya ndoto uliyonayo ni jambo la
muhimu sana. Kuwa na taarifa kunakusaidia kujua kwa undani hilo jambo kiasi
ambacho unakuwa na nguvu ya kukusaidia kulimiliki au kulitawala eneo hilo. (Information
is power).
Hili ni jambo ambalo hata tunaliona katika nyanja mbalimbali
za kisiasa, kielimu, kihuduma, kiuchumi na hata kiutamadumi, watu waliofanikiwa
ni wale walio na taarifa sahihi kulingana na maeneo hayo. Jitahidi kujijengea
tabia ya kupata taarifa sahihi kutoka kwa watu, nyaraka mbalimbali zilizotunzwa
kwa njia ya Vitabu, majarida hata sauti kwa njia ya Sauti. Hili jambo
lilimsaidia hata Danieli kujua ya kuwa Muda wao wa kukaa utumwani ulikuwa
umekwisha.....
" katika mwaka wa kwanza wa kumiliki
kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu,
nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii,
ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini"(Danieli 9:2)
Danieli alipata taarifa kwa kuvisoma vitabu, alisoma vitabu
gani (2Nyakati 36:21, Yeremia 25:11-12, yeremia 29:10)
IV). NGUVU YA MAOMBI.
Unapozungumzia
nguvu ya maombi ni jambo la msingi sana pia katika kujijengea uwezo binafsi wa
kuibeba ndoto ya Mungu katika maisha yako katika eneo ambalo Mungu amekupa.Kwa
njia ya maombi Mungu anazidi kuachilia maono katika hilo jambo,lakini pia Mungu
anatumia njia ya Maombi ili kukujengea "msuli wa ndani"
utakaokusaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali unapotembea katika ndoto
hiyo.Shetani asingetaka ujenge uwezo katika hilo jambo ambalo Mungu amekupa
kulifanya kwa hiyo kwa njia ya maombi unaweza kuziangusha ngome na kila fikra
zinazojiinua kinyume na mpango wa Mungu juu ya maisha yako.
Hebu
Tuangalie mifano hii michache.
Mfano wa kwanza.
Nehemia katika kuujenga ukuta wa
Yerusalemu na malango yake yaliyochomwa.
Unaposoma
kitabu chote cha Nehemia tunaona ya kuwa kusudi la Mungu juu ya Nehemia ilikuwa
ni kwenda kuujenga ukuta wa Yerusalamu pamoja na malango yake yaliyochomwa moto.
Hii haikuwa kazi Rahisi kwa sababu walikutana na upinzani mkubwa sana dhidi ya
Sanballat na Tobia. Lakini kilichomsaidia Nehemia ni kwamba alikuwa ana nguvu
ya maombi aliyoanza nayo kabla ya kuingia kazini.
"......Wakaniambia,
Watu wa uhamisho, waliosalia huko katika wilaya ile, wamo katika hali ya dhiki
nyingi na mashutumu; tena ukuta wa Yerusalemu umebomolewa, na malango yake
yameteketezwa kwa moto. Hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi,
nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, nikaomba mbele za
Mungu wa mbinguni"(Nehemia 1:3-4).
Nehemia akikutana na upinzani Dhidi
ya akina sanballat.....
"
Lakini ikawa, Sanbalati, na Tobia, na Waarabu, na Waamoni, na Waashdodi,
waliposikia ya kuwa kazi ya kuzitengeneza kuta za Yerusalemu inaendelea, na ya
kuwa mahali palipobomoka panaanza kuzibwa, basi wakaghadhibika mno; wakafanya
shauri wote pamoja kuja kupigana na Yerusalemu, na kufanya machafuko
humo"(Nehemia 4:7-8).
Kwa sababu ndani yake Nehemia
alikuwa amejijengea uwezo wa kukabiliana na changamoto hizo kwa njia ya maombi
aliyoanza nayo mwanzoni hakuiacha ndoto ya Mungu njiani, aliibeba mpaka pale alipomaliza.
"Basi huo ukuta ukamalizika siku ya
ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku hamsini na
mbili"(Nehemia 6:15).
Mfano wa pili.
Yesu alipokuwa Gethsemani akiomba
kuelekea msalabani.
Ndoto ya
Mungu juu ya Bwana Yesu ilikuwa ni Yesu kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu.
Lakini haikuwa kitu rahisi kwa Bwana Yesu kuibeba ile ndoto pale alipokuwa
akikaribia kwenda msalabani, aliingia kwenye maombi mazito kiasi cha jasho
misiri ya damu kumtoka, alipokuwa anakaribia kwenda msalabani (kuibeba ndoto ya
Mungu) alisema maneno haya ya kusema....
"
Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu,
ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali
kama utakavyo wewe"(Mathayo 26:39).
" Akaenda tena
mara ya pili, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki
kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatimizwe"(Mathayo 26:42).
"Akawaacha tena, akaenda, akaomba mara ya tatu, akisema
maneno yale yale"
(Mathayo 26:44).
Tunaposoma maneno hayo tunaona namna ambavyo Yesu alikuwa
amekosa ujasiri wa kulibeba kusudi la Mungu yaani kuelekea msalabani. Lakini
aliendelea kumwomba Mungu mahali pale na kupitia maombi yale Mungu alikuwa
akimtengenezea msuli wa ndani ili aweze kuibeba ndoto ya Mungu, na katikati ya
maombi yale Malaika akaja na kumtia nguvu (Kumwongezea uwezo wa kuibeba ndoto
ya Mungu) ...
"Malaika kutoka mbinguni
akamtokea akamtia nguvu. Naye
kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama
matone ya damu yakidondoka nchini"(Luka 22:43-44).
Je ni mara ngapi huwa unaingia katika maombi na kumwomba
Mungu kwa habari ya ndoto ambazo ameweka katika maisha yako, je unao ujasiri wa
kutosha wa kuiendea hiyo ndoto na kuifanya kuwa kiti dhahiri, jitahidi kukaa
katika maombi kwa muda wa kutosha ilim kujijengea misuli zaidi na ujasiri wa
kuibeba hiyo ndoto kwa utukufu wa Mungu.
V)
NGUVU YA UVUMILIVU. (The power of
perserverence).
Katika swala zima la kujijengea uwezo binafsi kwa ajili ya
kuibeba ndoto ya Mungu katika maisha yako uvumilivu ni jambo la msingi sana.
Unapokuwa katika hizo hatua kuna mambo mengine utakayokutana nayo na itatakiwa
kukabiliana nayo, vipingamizi, vikwazo, kuchukuliana na watu na hata wakati
mwingine unaweza kuanguka (ups and downs),
lakini jambo la msingi ni kuwa mvumilivu.
"Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani,
Bwana atakuwa nuru kwangu"(Mika 7:8).
" Hatua za mtu zaimarishwa na Bwana, Naye
aipenda njia yake. Ajapojikwaa hataanguka chini, Bwana humshika mkono na
kumtegemeza"(Zaburi 37:23-24).
Kitu gani
nataka tuone pamoja kwenye hiyo mistari ni kuwa katika safari yoyote ya
kuelekea kwenye ndoto yako kuna kuanguka lakini hii isikukatishe tamaa kama
mika anavyosema hapo juu kuwa "niangukapo
nitasimama tena”, lakini pia wakati mwingine unaweza kujikwaa katika baadhi
ya mambo uwe na uhakika ya kuwa Mungu atakusimamia na kukupigania mpaka pale
ndoto hiyo itakaposimama kama Muimba Zaburi anavyosema kuwa "Bwana humshika mkono na kumtegemeza"
Swala la
kujijengea uwezo ni mchakato (Process) na si jambo la siku moja
tu (an
overnight process), hivyo linahitaji kujitoa kikamilifu kabisa, Mungu
atakuchukua hatua kwa hatua ili kuiendea ile ndoto aliyoiweka katika maisha yako.
Mungu anafanya kila jambo kwa wakati maalumu kwa hiyo hata anapokupitisha
darasani kwa ajili ya kukujengea uwezo huo anajua unahitaji kukaa katika hilo
darasa kwa muda gani.
Mungu alimwambia Habakuki maneno
haya...
"Maana
njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia
mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia,
ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia"(Waebrania 2:3).
Kwa maneno
hayo Mungu alikuwa akizungumza na Habakuki kwa habari ya kuwa mvumilivu
kusubiri kwa maana ile ndoto ni kwa wakati ulioamriwa.
MAENEO
MUHIMU/AINA YA UWEZO UNAOWEZA KUJIJENGEA
v
Uwezo wa Kuitambua ,kuisikia sauti
ya Mungu…kwa bidii
v
Uwezo wa kukiatamia kile kitu Mungu ameweka
katika maisha yako (Kuliatamia yai ambalo Mungu ameweka kwenye maisha yako ili
utotoe kifaranga-an ability to incubate)
v
Uwezo wa kubadili mfumo wako mzima
wa kufikiri (Gods plan versus your plan….Yeremia, Gideoni)-Ability to remove
the inferiority complex
v
Ability to resist bad news……. Taarifa
gani unaisikia na ni kwa wapelelezi gani??
v
Uwezo wa kufanya kazi kama team
v
Uwezo wa kuwachukulia watu na
madhaifu waliyonayo…Eg. Jesus versus petro
v
Uwezo wa ku-Master eneo ambalo Mungu
anataka umtumikie
v
Uwezo wa ku-handle failure
v
Uwezo wa ku-handle success
v
Uwezo wa kuvumilia na kuzitazamia
ahadi za Mungu
v
Uwezo wa kutunza siri mbalimbali za
Mungu
v
Uwezo wa kuwa na utulivu wa Rohoni
na kuisubiri saa ya Bwana
v
Uwezo wa kuwa na ufahamu juu ya
majira na nyakati na kujua mambo ya msingi unatakiwa kufanya kwa kuzingatia
majira na nyakati hizo.
Nakutakia
mafanikio mema pindi unapoendelea kujijengea uwezo wa kulibeba kusudi la Mungu katika
maisha yako, niseme tu kwamba Mungu analokusudi kubwa sana juu ya hiyo ndoto aliyoiweka
katika maisha yako, wako watu wengi sana huku wanasubiri kuvuka mahali waliko
kwa kufanikiwa kwako wewe katika ndoto hiyo/kusudi hilo, yaani ndoto hiyo
imebeba pia maisha ya watu wengine, jifunge mkanda, simama kikamilifu. mlingane
Mungu na uudhihirishie ulimwengu thamani ya ile ndoto Mungu ameiweka katika
maisha yako kwa utukufu wa Mungu. Inawezwekana kwa
yeyote aliye tayari kulipa gharama ili kuifanikisha.
Japokuwa kuna ghrama katika kujijengea uwezo na kuibeba kusudi la
Mungu, lakini ipo neema ya kumsaidia kila mmoja katika eneo lake.
Wako
katika kuujenga Mwili wa KRISTO(Kanisa)
Mwl.Musa
Festo
Mungu
akubariki kwa viwango vya juu.
Contacts:
0675415262.
mussafesto@gmail.com.
Comments
Post a Comment