SOMO: MAOMBI YA KUFUNGA.
UTANGULIZI.
Maombi ni muhimu sana kwa Mkristo
aliyeokoka kwani maombi ni SILAHA.Tutazame maombi ya kufunga katika vipengele
vikuu vitano
1 Kwanini tunafunga
2 Siku za
kufunga 3 Faida za maombi ya kufunga
4 Hasara za kutokufanga 5 Kuisikia
sauti ya Mungu
1.
KWANINI TUNAFUNGA?
Tunafunga ili kuisikizisha sauti yetu
juu, kwa maneno mengine tunafunga ili kusikiwa na Mungu zaidi. Tunafunga ili
kufungua vifungo vya uovu ambavyo vimeshindikana kwa maombi ya kawaida. Tunafunga
ili kujinyenyekeza kwa Mungu kupata nguvu na Neema. Tunafunga ili kupata majibu
ya haraka kwa mambo magumu. Tunafunga pia kwasababu maombi ya kufunga ni maombi
yanayomgusa Mungu na kuvuta uwepo na nguvu zake hasa katika huduma. Tufunga pia
ili kupata nguvu ya kuungamanisha Imani zetu kwa Mungu.
Danieli 10:1-3. 1 Katika mwaka wa
tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danieli, ambaye jina lake aliitwa
Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni vita
vikubwa; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo. 2 Katika siku zile
mimi, Danielii, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili. 3 Sikula chakula
kitamu, wala nyama wala, divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka
mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia.
Katika Danieli 9: 2 Danieli baada ya kuvisoma vitabu alifahamu hesabu ya
miaka ambayo Mungu alikuwa amemwambia nabii Yeremia kuhusu Taifa la Israeli
kuutimiza ukiwa Wa miaka Sabini. Danieli 9:3. Ndipo nikamwelekezea Bwana uso
wangu, ili kutaka kwa maombi,na dua,pamoja na kufunga na kuvaa nguo za magunia
na majivu. Bila shaka miaka
ya kutolewa kwa taifa hili utumwani ilishatimia na kupita lakini hakuna
aliyeona wala kutia akili, bali watu waliendelea na uovu wao mpaka hapa Danieli
anapokuja kupitipitia vitabu anagundua hili jambo ambalo Mungu alikuwa
ameshalitamka, inawezekana wakati wako wa kutoka utumwani ulishafika muda mrefu
na tayari umeshapitiliza lakini kwa kuwa hujajua njia za kutoka hapo kwa
kuutafuta uso wa Mungu kwa kufunga na kuomba bado umeendelea kufungwa katika
kifungo hicho, Yesu aliwaambia wanafunzi wake katika Marko 9:29; Namna hii haiwezi
kutoka kwa neno lolote,isipokuwa kuomba, Ingia katika maombi ya kufunga ili kufungua na kuvunja hiyo
nira,kama tulivyojifuza kazi ya maombi haya ya kufunga ni kuleta majibu ya
haraka kwa mambo magumu,pia kuifanya sauti yako kusikiwa na Mungu na kupeleka
Msaada wake wa haraka kwa mambo magumu, Esta, anaiingia katika Maombi ya siku
tatu, yeye pamoja na vijakazi wake pamoja na Israeli wote, ili apate kibali kwa
mfalme kinyume cha sheria, na Mungu alipeleka Msaada Wa haraka kupitia maombi
ya kufunga akapata kibali kwa mfalme badala ya kuuwawa, mfalme akamnyoshea
fimbo yake ishara ya kumkubali, Maana kama ingetokea mfalme asingemnyoshea
fimbo yake basi kwa sheria za Mfalme AhasueroEsta angeuwawa kwani aliingia
kinyume cha utaratibu. Esta 4:11, Watumwa
wote Wa Mfalme, wanajua sana, hata na watu Wa majumba ya mfalme, ya kwamba mtu
yoyote, akiwa mwanaume au mwanamke atakeyemjia mfalme katia uwa Wa ndani, wala
hakuitwa kuna sheria moja kwake nayo ni kwamba auawe. Maombi ya kufunga yana
uwezo Wa kukupenyeza mahali ambapo kwa hali ya kawaida usingepenya, yana uwezo
wa kukuketisha na watu au mahali pa juu, mahali ambapo kwa elimu yako
usingestahahili kuketi.
KIPENGELE CHA 2
SIKU ZA KUFUNGA: Ziko aina mbali mbali za kufunga Ila Mimi nitazungumzia aina kumi.
a.
Aina yetu ya kwanza ni kufunga kwa kuvusha mlo mmoja kwa mtu aliyezoea
kula Milo mitatu kwa siku anatakiwa kuacha kula mlo mmoja.
b.
Funga ya pili,kuvusha milo miwili saa 24 ,unaacha kula asubuhi na mchana
unakula jioni hii ndio funga ambayo watu wengi huependelea kufunga.
c.
Kuvusha Milo mitatu yaani moja, kavu saa 24.
d.
Kuvusha Milo sita yaani mbili kavu saa 48.
e. Kuvusha Milo 9,tatu kavu masaa
72,,,,,,,,,,,,, ,=",-,: ,(,, ,, ,, 0);",Hii ndio funga aliyoifanya
Esta, Esta 4:16 Uende ukawakusanye
wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwaajili yangu,msile wala
kunywa,muda wa siku tatu,usiku na mchana,nami na wajakazi wangu tutafunga vile
vile,kisha nitaingia kwa mfalme,kinyume cha sheria,nami nikiangamia na
niangamie.
f.
Funga ya Danieli, kutokula vyakula vitamu, ,;Danieli alifunga kwa kula
mtama na maji ,;Alifunga muda Wa majuma matatu, siku 21.
Danieli 10:2-3 Katika siku zile, Mimi
Danieli nilikua nikiomboleza muda Wa majuma matatu kamili, Sikula chakula
kitamu, wala nyama wala divai haikuigia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta
kabisa hata majuma matatu kamili yalipotimia.
g.
Funga ya Yohana Mbatizaji, Alifunga kwa kula chakula cha aina moja tu
nzige na asali.
h.
Funga ya kulazimishwa hii ilimtokea Yona. Hapa Ni Mungu mwenyewe huhusika
kumfungisha mtu/watu kwa kusudi lake mwenyewe Yona 1:17 Kisha Mungu akaamuru
samaki mkubwa ammeze Yona,naye akawa tumboni mwa Samaki huyo kwa muda Wa siku
tatu,usiku na mchana. Pia katika Matendo 27:33. Karibu na alfajiri,Paulo
aliwahimiza,wote wale chakula" Kwa siku kumi na nne sasa mmekuwa katika
Mashaka na bila kula,hamjala
kitu chochote. Kuna watu ni waoga kufunga, wakati mwingine Mungu hutumia
njia mbadala kama ya Yona na kina Paulo ili kuwafundisha kufunga.
i.
Funga ya Musa na YESU ya siku 40
j.
Funga ya Hadhara au Taifa zima au kanisa zima. Mfano wa funga hii Ni
wakati wa Corona Raisi wetu John Pombe Magufuli alitakaza maombi ya kufunga ya
Taifa kwa muda wa siku tatu ili Mungu alinusuru taifa Letu na janga la Corona. Lazima
funga ziwe siri na zifungwe kwa unyenyekevu mkubwa, unapofunga mtu yoyote asijue
isipokuwa wewe na Mungu, labda iwe ni funga ya hadhara tena kama ni kanisa basi
iwe siri kwa kanisa husika hata kanisa jingine lisifahamu, hii ni kwa sababu Biblia
inasema katika Mathayo Sura ya,;6:16 Tena mfungapo msiwe kama wanafiki,wenye uso wa
kukunjamana,maana hujiumbua nyuso zao,ili waonekane na watu kuwa
wanafunga,Amini nawaambia wamekisha kupata thawabu yao, Bali wewe ufungapo
jipake mafuta kichwani,unawe uso,ili usionekane na watu kuwa unafunga,Ila na
Baba yako aliye sirini,na Baba yako aonae sirini atakujazi. Lazima
funga ifungwe kwa furaha ya Roho Mtakatifu na sio kulazimishwa. Lazima funga
iambatane na maombi. Tafuta muda mzuri Wa kuwa na utulivu na Mungu. Funga inakuwa
na nguvu mtu anapoomba la sivyo unakuwa umekaa na njaa bure na kuuchosha mwili
tu. Lazima funga iambatane na Upendo na sio ubinafsi, Hakikisha unapofunga
unawapa wengine chakula chako, ambacho ungekula mchana. Isaya 58:6 Kufungua vifungo vya
uovu, kuzilegeza kamba za nira,kuwacha huru walionewa,kuwagawia wenye njaa
chakula chako na kuwaleta masikini waliotupwa nje nyumbani kwako,Umwonapo mtu
aliye uchi,umvike nguo,wala usijifiche na mtu mweye Damu moja nawe. Uko
tayari kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria kudai haki yako?
Basi chukua hatua ya maombi ya kufunga.
KIPENGELE CHA 3 FAIDA ZA KUFUNGA. Isaya 58:8-11… 8 Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama
asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa
Bwana utakufuata nyuma ukulinde,
9 Ndipo utaita, na Bwana ataitika;
utalia, naye atasema, Mimi hapa. Kama ukiiondoa nira; isiwepo kati yako, wala
kunyosha kidole, wala kunena maovu; 10 na kama ukimkunjulia mtu mwenye njaa
nafsi yako, na kuishibisha nafsi iliyoteswa; ndipo nuru yako itakapopambazuka
gizani; na kiwi chako kitakuwa kama adhuhuri, 11 Naye Bwana atakuongoza daima,
ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji na kuitia nguvu mifupa yako;
nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji na kama chemchemi ambayo maji yake
hayapungui.
Faida ya kwanza kulegeza kamba za
nira. kama kuna vifungo vigumu vinafunguliwa. Nuru yako itapambazuka kama
asubuhi, ukifunga wakati dunia inatembea katika Giza wewe uyefunga nuru ya
Mungu inapambazuka. Isaya 60:1 Ondoka, uangaze kwa kuwa nuru yako imekuja maana Giza
litaifunika dunia,na Giza kuu litazifunika kabia za watu, Bali Bwana atakuzukia
wewe na utukufu wake utaonekana kwako.
Utapata haki zako bila kupigania, hutatafuta
haki itakufuata ulipo. Kiu yako itakua adhuhuri, Giza lililokiwa kwako litakuwa
nuru.
Utaponywa afya yako na mifupa yako
itatiwa nguvu.
Funga huleta uponyaji. Bwana atakuwa
kiongozi wako daima, utukufu Wa Mungu utakutangulia mbele ukulinde. Mungu
ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji.
Mungu atakufanya uitwe heri. Utukufu Wa Mungu utakufuata nyuma ukulinde daima.
KIPENGELE CHA 4. HASARA ZA KUTOKUFUNGA
1. kuna baadhi ya mambo hatawezekana
Kwenye maisha yetu ya Kiroho. Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila
kwa kusali na kufunga.]
2. Kazi ya Mungu itakuwa ngumu bila kuwa
na maombi ya kufunga. Ndiyo maana Yesu aliye kielelezo chetu kabla ya kuanza
kazi yake aliyotumwa na Mungu alianza kwa kufunga na kuomba.
3.
Nguvu za Kiroho zinakuwa kidogo na wakati wa Majaribu ujapo moyo huzimia
Na kushindwa kustahimili. Mithali 24:10 Ukizimia siku ya taabu, Nguvu
zako ni chache.
4. Na tunapata nguvu za Mungu au nguvu
za Kiroho kupitia maombi ya kufunga na kuomba.
5. Huduma haitakua, utadumaa Kiroho,
6. Mwili utaishinda roho. Maombi ya
kufunga huutaabisha mwili na kuuthibiti ili utulie roho iyafanyayo mapenzi ya
Mungu ipate kutawala. Marko 14:38 Kesheni mwombe, msije mkaingia
majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.
7.
Bila maombi ya kufunga kazi ya Mungu itafanyika kwa ulegevu na kuifanya
kazi Mungu kwa ulegevu mwisho huleta laana katika maisha yetu kwa ujumla. Yeremia
48:10 Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya BWANA kwa ulegevu; na alaaniwe auzuiaye
upanga wake usimwage damu.
KIPENGELE
Maombi ya kufunga hutuweka karibu
sana na Mungu wetu na hutufanya kuisikia sauti ya Mungu wetu kwa kila jambo
atuagizalo au anapotoa majibu yetu na hufanya tumwone Mungu.
Mfano Danieli baada ya kufunga na
kuomba siku 21 sauti ya Mungu ilisikika kwake kwa ujumbe wa malaika. Danieli
10:2 Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma
matatu kamili. 3 Sikula chakula kitamu, wala nyama wala ,ai haikuingia kinywani
mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia. 4
Na siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa kando ya ule mto
mkubwa, Hidekeli; 5 naliinua macho yangu, nikatazama, na kumbe, mtu aliyevikwa
nguo za kitani, viuno vyake vimefungwa dhahabu safi ya Ufazi; 6 mwili wake pia
ulikuwa kama zabarajadi safi, na uso wake mfano wa umeme, na macho yake kama
taa za moto, na mikono yake na miguu yake rangi yake kama shaba iliyosuguliwa
sana, na sauti ya maneno yake kama sauti ya umati wa watu. 7 Nami, Danieli,
nikaona maono haya peke yangu; maana wale watu waliokuwa pamoja nami
hawakuyaona maono haya; lakini tetemeko kuu liliwashika, hata wakakimbia ili
kujificha. 8 Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala
hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa
uharibifu, wala sikusaziwa nguvu. 9 Walakini naliisikia sauti ya maneno yake;
nami niliposikia sauti ya maneno yake, ndipo nikashikwa na usingizi mzito, na
uso wangu umeielekea nchi.
Maombi ya kufunga huushinda mwili na
kuufisha na kufanya masikio yetu ya ndani kusikia mwito wa Mungu na macho yetu
ya Kiroho kutiwa nuru.
Wagalatia 5:17 Kwa sababu mwili
hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi
zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. Waefeso 1:18 macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito
wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu
jinsi ulivyo.
Mungu akubariki kwa viwango vya juu!!.
Mwl. Musa Festo
Contacts: mussafesto@gmail.com
+255675415262.
#SalsalaPenyeMaziwanaAsali
Comments
Post a Comment