SOMO: UWAKILI
ANDIKO LA MSINGI 1
WAKORITHO 4:1.
Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa
Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. Hapo
tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu
UTANGULIZI.
Wakili ni nani: Ni msimamizi wa kazi au shughuli za
mtu mwingine, ni mtetezi na mwangalizi.
Pia Wakili ni mwakilishi
Kwa hiyo Uwakili Ni
kitendo cha mtu kusimamia kazi au shughuli za mtu mwingine na kuwa mwangalizi
wa mtu mwingine, Pia ni kutekeleza jambo au kazi kwa niaba ya mtu mwingine
Huo ndio Uwakili
Kwa neno lingine naweza Sema Uwakilishi
Kazi za wakili
· Kumtambulisha
yule anaye muwakilisha. (Tumevaa sura ya Kristo…Math. 26:73).
·
Kuhakikisha
shughuli aliyopewa kusimamia inaenda jinsi alivyopanga Yule anayemwakilisha.
Yesu anaweka wazi juu ya hali pale anapamwambia Baba yake(Mungu) juu ya kazi
aliyomtuma duniani yaani kumwakilisha Mungu duniani na kumtukuza.(Yohana 17:4).
·
Kuwa
mtetezi wa yule anaye mwakilisha
·
Kufanya
kazi kama ambavyo angefanya mwakilishi wake. N.k
Wakili hawezi kufulahi kuona shughuli ya Bwana wake
inadharauliwa na haifanikiwi katika kiwango kusudiwa bali Atatumia bidii yake
kuhakikisha inaenda vizuri....
Wakili huwa ana act kama Bwana wake. Anafanya yale yote ambayo
Bwana wake angeyafanya Tena Kwa ustadi mkubwa
Huyo Ndiye Wakili mwema anayejua kazi yake.
Nimekupitisha huko ili uone jinsi Wakili alivyo lakini leo nataka
tumzungumzie Wakili wa Kristo.
Wakili wa Kristo ni nani?
Kila aliyemwamini Kristo na kumpokea anafanyika kuwa
Wakili wa Kristo .Hivyo wewe uliyeokoka ni Wakili wa Kristo Na umefanyika kuwa shahidi wa Kristo
Duniani
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia
juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na
katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. Matendo ya Mitume 1:8
Uliyemkristo unafanyika kuwa shahidi (Wakili) wa Mungu katika
ulimwengu. Umepewa kusimamia Kazi au shughuli na Mali za Mungu Unatakiwa
kuushudia uhalisia wa Mungu Kwa Mataifa yote.
Sasa shida ipo hapo kwenye kuuishi
Uwakili wetu. Shetani
ametuvuruga na kutuingizia mambo Mengine mengi ambayo hayafanani na yule
tunayemuwakilisha wala hayatoki kwake na tumeacha kufanya yaliyotupasa
kuyafanya.
Yapo mengi shetani aliyoyahalalisha kwetu tuyaone kuwa ni Sawa
Kumbe si Sawa balada ya kumwakilisha Mungu tunamdhalilisha Mungu wetu.
Wakili wa Mungu anapaswa kufanya yale mambo ambayo
Mungu anataka kuyafanya Duniani
Kwa hiyo anafanya Kwa niaba ya Mungu(
Mungu ni Roho hawezi kushuka duniani na
kuihubiri injili na kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wake ila ametupa sisi
tulio milki yake kazi hiyo hapa duniani kama Mawakili wake yaani tunatenda kazi
kwa niaba yake). Kama mawakili tunapaswa kupitisha Mapenzi ya Mungu Duniani
ufalme wa Mungu ujulikane Duniani kupitia sisi.
Kwa mfano tumeuona Upendo wa Mungu juu ya watu wake hadi anamtoa
wanawe wa pekee afe Kwa ajili ya watu wake
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda
ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali
awe na uzima wa milele. Yohana 3 :16
Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni
ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Yohana 3 :17
Kwa hiyo ni kazi ya Wakili kuuendeleza Upendo ambao Mungu
ameuanzisha Duniani. Maana Yesu anasema yeye ndiye njia kweli na uzima hivyo
yatupasa kupita katika yeye tena anasema twaeni nira yangu mkajifunze kwangu…….. Sasa cha kushangaza Sisi tulio mawakili
badala ya kudumisha Upendo Sisi tunazidi kuupoteza
Pia Tunaona lengo la Mungu kumtoa mwanawe wa pekee ni ili
ulimwengu uokolewe
Kwa hiyo ni kazi ya Wakili kuhakisha wanadamu hawapotei bali wanaokolewa kama
vile Mungu alivyo kusudia.
Hebu tuone jinsi Wakili wa Mungu
anapaswa kufanya
1. Wakili
napaswa kumjua Mungu na kuzitambua siri za Mungu.
1 Kor 4:1.Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi
wa Kristo, na mawakili
wa siri za Mungu. Hapo tena inayohitajiwa katika
mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu
Kwanza kabisa ili uwe wakili wa Mtu Fulani ni lazima na muhimu
kumfahamu vyema mtu huyo unayemtetea na kujua undani wake na jambo husika. Ni
jambo la ajabu sana kumtumia Wakili katika kesi asiyejua sheria vizuri na
vifungu vya sheria na hajui undani wa kesi yako, ni wazi kabisa hataweza
kukutetea na mwisho utashindwa katika kesi yako hata kama uwezekano wa kushinda
ulikuwepo.
Na sisi kwa sababu tu Mawakili wa Mungu tena Mawakili wa siri za
Mungu ni lazima tumjue Mungu kwa undani sana na kuzitambua vyema siri za Mungu.
Tuwezaje kumjua Mungu na siri zake?
·
Kupitia Neno lake. Tunamjua Mungu kupitia
Neno lake kwani maandiko yanasema amejifunua
kupitia Neno lake. Ndiyo maana Mandiko yanasema katika Wakolosai 3:16 “Neno la
Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na
kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa
neema mioyoni mwenu.
·
Tunaweza zijua siri za Mungu Kupitia Roho
wake (Roho Mtakatifu).
Ili kuzijua siri za Mungu kama Mawakili wa Mungu lazima ndani
yetu tuwe na Roho Mtakatifu kwani huyu ndiye pekee afunuae hata mafumbo ya
Mungu na kutujulisha maana ni Mungu halisi. 1 Wakoritho 2:10 “Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho
huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu”.
Huyo Roho akiwa ndani yetu Utumishi
wetu na Uwakili wetu wa siri za Mungu unakamilika nasi tunakamilishwa naye
na kufikia utu uzima wa kufikia kima cha
kumlingana Kristo YESU.
2. Kumtambilisha
Mungu Kwa Mataifa
Wakili wa Mungu ni kitambulisho cha Mungu. Kwa maana hiyo popote
atakapo ingia wajue kuwa Mungu yupo mahali hapo. Ni lazima Wakili afanane na
Mungu katika Utendaji, Watu wamuone Mungu ndani yake katika matendo (life style)
yake yote yawe na utambulisho wa Mungu. Watu waamini kuwa Mungu Yupo na
anatenda kazi kupitia Yeye.
3. Kuhakikisha
shughuli aliyopewa kusimamia unafanyika vile ilivyokusudiwa
angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa
na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili
kujenga na kupanda. Yeremia 1:10
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote
kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na
kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja
nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. Mathayo 28 :19-20
Hiyo Ndio Kazi kubwa tuliyopewa Mawakili Kwa hiyo Wakili lazima
ahakikishe hayo yote yanatukia jinsi ilivyokusudiwa. Ndiyo maana mtume Paulo
anasema katika 1 Kor 4:1. Mtu na atuhesabu hivi,
kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. Hapo
tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu. Maandiiko yanaweka wazi lazima Wakili awe
mwaminifu.
4.
Kuutete Ufalme wa Mungu. Wakili anapaswa kusimamia na kuutea
ufalme wa Mungu na kutokukubari kuona ufalme wa Mungu unadhalilishwa na
kuonekana si kitu Duniani
Bali Wakili atasimama na kuhakikisha ufalme wa Mungu unajulikana
5. Kufanya
Kazi Kama Ambavyo Mungu anataka ifanyike au Kufanya yale Mungu aliyoyakusudia
Duniani.
Yesu alikuwa na huruma aliwahurumia Mataifa akawapa chakula, akawaponya, akawafufua
In short alifanyika msaada Kwa watu alikuwa utatuzi Kwa matatizo ya watu N.k
Hivyo Wakili anapaswa kuyadumisha hayo yote kama Mungu alivyokusudia.
HITIMISHO
Kanisa lililo mwili wa Kristo ni Wakili wa Kristo hivyo linapaswa kuyaishi maisha hayo
na Mengineyo ambayo Mungu amelikusudia Kanisa liyaishi na liwe kimbilio la watu. Watu
wakimwitaji Mungu wakimbilie kanisani wakutane na Mungu na kutatuliwa shida zao.
Sasa Ebu tujiulize je Kanisa la leo linayaishi maisha hayo katika kiwango kusudiwa?
Wewe uliye Mkristo na kuhani - yaani mpatanishi wa watu na Mungu kwani Kuhani maana yake ni Mpatanishi wa watu na Mungu kama alivyo Kristo Je unayaishi maisha hayo?
Kama ndiyo Mungu na azidi kukupa Neema
hiyo na kukubariki kwa viwango vya juu na kama siyo basi anza upya fufua uamsho ndani yako na kurudi katika
nafasi yako ya UWAKILI.
MUNGU AKUBARIKI KWA VIWANGO VYA JUU.
Mwl. Musa Festo
Contacts: mussafesto@gmail.com
+255675415262.
#SalasalaPenyeMaziwanaAsali
Comments
Post a Comment